KULETWA KWA MIILI YA WANAJESHI 7 WATANZANIA WALIOFIA DARFUR BADO HAIJAJULIKANA


Photo: Natuma salamu za pole kwa amiri jeshi mkuu,ndg za marehemu na wanajeshi wote kwa msiba huu mkubwa uliotukuta.Wamekufa wakiwa kazini wakitekeleza majukumu yao ya kazi.Mungu awape moyo wa subira na uvumilivu wananchi,wanajeshi wote na wafiwa.R.I.P MAKAMANDA WETU.

Jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ limesema linasubiri matokeo ya uchunguzi wa Umoja wa Mataifa juu ya kikundi kilichohusika pamoja na mazingira ya mashambulizi yaliyosababisha kuuawa kwa wanajeshi 7 wa Tanzania wanaolinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan.

Akizungumza kupitia Kipindi cha Hot Mix kinachorushwa na EATV, msemaji wa jeshi hilo Kanali Kapambala Mgawe amesema jeshi linasubiri ripoti ya umoja wa mataifa ili kuamua ni lini miili ya marehemu italetwa nchini, 

Aidha amekanusha juu ya taarifa zilizo sambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Jeshi hilo limetoa majina ya wale waliofariki katika shambulio hilo

"Kuna baadhi ya majina tume yaona kwenye vyombo vya habari lakini sisi hatukutoa majina ya wale walio uwawa, Jeshi lina utaratibu wake katika matukio kama haya sijui haya majina nani kawatajia, hivyo siwezi kusema ni nani ameuwawa kwani majina bado hayaja wekwa hadharani" amesema

Kanali Kapambala Mgawe amesema, utaratibu wa kijeshi nikuwa mtu anapo uwawa, nilazima ndugu wakaribu waambiwe kwanza na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo nasio kutamka kwenye vyombo vya habari kwani inaweza kusababisha matatizo mengine.

Mtu amefiwa na mtuwake wa karibu wewe unatoa jina lake, je atajiskiaje kusikia kwenye vyomboi vya habari bila kuambiwa kwa utaratibu unao faa, Alihoji na kueleza kuwa kilicho tendeka sio utaratibu mzuri kwani wao ndio walipaswa lutoa taarifa kwa ndugu wa marehemu. Alisema Kanal Kapambala

Amesema kwa hivi sasa jeshi hilo halina mpango wowote wa kuongeza wanajeshi nchini Sudani kwani walioko wanatosha lakini endapo watatakiwa na umoja wa mataifa kufanya hivyo wataongeza.

Jumla ya wanajeshi 875 walikuwa nchini humo tangu mwezi February mwaka huu, kwa maana hiyo walio hai mpaka hivi sasa ni 868 (ukitoa 7 waliofariki) na miongoni mwa hao walio hai 14 walijeruhiwa na wapo katika hali mbaya
.Wanajeshi hao walishambuliwa wakati wakisindikiza msafara wa waangalizi wa amani wa Umoja wa Mataifa, Tangu Tanzania ianze kupeleka majeshi yake mwaka 2007 huko Darfur ni mara ya kwanza kwa Jeshi letu kupoteza watu wake. Pole Tanzania Pole kwa ndugu jamaa na marafiki walioguswa na msiba huu.


EmoticonEmoticon