VIKOBA SASA YAFIKISHA KIASI CHA BILLIONI 300 BENKI, RAISI WAO AFURAHIA MAFANIKIO

Rais wa Vikoba Tanzania na Mbunge wa Viti maalum kupitia tiketi ya CCM Bi. Devota Likokola amesema hivi sasa katika benki vikoba imefikisha kiasi cha Shilingi Billioni 300 kiasi ambachi kitawasaidia kuinua mitaji mbalimbali ambayo Vikoba inalenga kufanikisha 


Aidha ameongeza kuwa kuna watu wengi wanapenda kujiunga katika vikoba lakini nafasi inakuwa finyu kwani muamko umekuwa mkubwa sana baada ya watu wengi kuona mafanikio wanayopata katika Vikoba. amesema Devota

Baadhi ya makundi yaliyopo kwenye vikoba yamefanikiwa kutengeneza bidhaa zao licha ya kuwa na changamoto nyingi ikiwa pamoja na Vifungashio za bidhaa zao


Hizi ni bidhaa ambazo zimetengenezwa na kikundi cha MAONO GROUP - MAVURUNZA wanatengeneza bidhaa kama Asali, Dawa ya Maleria na Tea Masala,Sabuni na nyingine nyingi kwa mawasiliano zaidi piga simu 0754 616779 ilikupata bidhaa za chama hicho


Wanachama wa chama hicho ni Neema Mbazi, Rebeka Masuki, Hilda Msuya, Juliana Marando, Aisha Mbwana, Martha Moris, Ruth Changa.



Chama kingine ni Better Life ambacho kimeweza kutengeneza bidhaa kama shampoo, sabuni ya vyombo na sabuni ya chooni, dawa ya Deto, dawa ya kuweka hewa safi, dawa ya kuoshea Ditels na vingine vingi


Better Life ina wanachama wengi zaidi ya 10 na wato wanashirikiana ilikuweza kumudu garama za uzalishaji pamoja kusambaza bidhaa zao kwa lengo la kujipatia fedha



EmoticonEmoticon