WAZIRI MKUU WA TANZANIA ARUHUSU POLISI KUPIGA RAIA

Photo: HOTMIX (11:00 Jioni) Polisi wakabidhiwa rungu, watakiwa kushusha kichapo kwa kila mtu atakaye waletea ubishi... Hiyo ni kauli kutoka kwa Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda leo Bungeni, Una maoni gani kuhusu hilo?

Pia, tuko na mkemia mkuu wa serikali, Je, unajua ni perfume na deodorant za aina gani zinazoweza kukusababishia kansa? Uliza maswali yote yanayohusu vipodozi, perfume, DNA na dawa mbalimbali utapata majibu HAPA!

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda amewakabidhi rungu Jeshi la Polisi ilikupiga raia ambao watajikusanya au kuandamana bila kibali cha Jeshi hilo

Akijibu maswali ya papo ka hapoambayo huyajibu kila Alhamisi Bungeni, Waziri mkuu huyo amesema Polisi wapige tu raia wakati akijibu swali lililo ulizwa na Mbunge wa Kilwa Mhe. Murtaza Mangungu aliye taka kujua serikali inachukua hatua gani kwa Polisi wanao piga raia

Mhe. Pinda alijibu kuwa,
“Ukifanya fujo na umeambiwa usifanye hiki na ukafanya fujo na ukakaidi ukafanya fujo  utapigwa tuu, hakuna maana nyingine, nilazima tukubaliane kuwa nchi hii ina endeshwa na misingi ya kisheria  sasa kama wewe umekaidi hutaki unaona kama nijeuri na zaidi wewe ndio jeuri zaidi utapigwa tuu na mimi nasema wapigeni tuu maana hatuna namna nyingie” alisema kwa msisitizo waziri huyo

Waziri mkuu aliongeza kuwa, Mara ya mwisho hapa Bungeni nilisema nataka kurudisha hali ya amani na nilisema nilazima turudishe amani sasa tuache tusiwakamate wakati wanavunja amanani, nyiye wenyewe mtasema tunawaachai” Alisema

Aidha Kauli hiyo ya Waziri iliyosindikizwa na makofi ya Wabunge… ilikuwa tofauti kwa Mbunge wa Konde Mhe. Khatibu Saidi Hadji aliyetaka Waziri huyo kujibu ni kwanini amevunja katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 13 kifungu cha 6-B na 6-E

Kifungo hichi kinasema kuwa, NIMARUFUKU KWA MTU YEYOTE ALIYESHATAKIWA KWA KOSA LA JINAI KUTENDEWA KAMA MTU MWENYE KOSA HILO, NI MARUFUKU KWA MTU YEYOTE KUTESWA, KUADHIBIWA KINYAMA AU KUPEWA ADHABU ZINAZOTWEZA UTU NA KUMDHALILISHA jambo ambalo Waziri alijibu kama ifuatavyo

Waziri mkuu alijibu kuwa, Lazima uweke tofauti kwa mtu aliye kamatwa na mtu ambaye anavunja sheria, kama wewe umeambiwa usiende kufanya maandamano ukaenda nilazima tufanye hivyo, na nilazima utii sheria bila shuruti. Alisema Mhe Pinda

Kwa muda sasa kumekuwa na taarifa hasa maeneo kunakotokea maandamano na vurugu, Raia kulalamikia polisi kuwa piga hata kuwa teas… ambapo Waziri mkuu kawakabidhi rungu kuwapiga raia

 Naogopa jamani nahisi kama bado kidogo hakuta kucha TZ



EmoticonEmoticon