RASIMU SIYO YA SIASA TU, TUJADILI NA MAPENDEKEZO MENGINE,LHRC YASEMA


Mashirika mbalimbali yanayohusika na utetezi wa haki za binadamu yameipongeza tume ya Katiba kwa kuweka kipaumbele katika suala la haki za binadamu katika rasimu ya katiba mpya iliyozinduliwa hivi karibuni.

Wakizungumza na Blog hii leo jijini Dar es salaam, mratibu wa katiba kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu Bi Anna henga pamoja na Mratibu kutoka mtandao wa Mashirika ya haki za binadamu kusini mwa Afrika bi Martina Kabisama, wamesema pamoja na mazuri yaliyomo kuhusu haki za binadamu, tume ya katiba inatakiwa kuliangalia upya suala la adhabu ya kifo.

Mtu anahaki ya kuishi, kuendelea kuwepo kwa kifungu kinachoruhusu adhabu ya kifo kwakeli nikinyume cha haki ya kila mtu kuishi, hivyo tunaliangalia zaidi hilo swala la adhabu ya kifo ambayo imependekezwa kwenye rasimu hii ya sasa” Alisema Anna Henga

Wanaharakati hao pia wamesema kuwa muda wa miezi miwili uliobaki kuelekea bunge la katiba hautoshi kwa wananchi kuielewa rasimu hiyo na hapa wanatoa mapendekezo.

Muda uliotolewa kuchambua rasimu hii kwa wananchi ni mdogo sana, kutokana na mambo yote kuwagusa moja kwa moja lakini kwa sisi wanaharakati au asasi mbalimbali ni rahisi kwani utaanza kusoma hasa kipengele kinacho kuhusu tu nakukitolea maamuzi haraka, Alisema Anna Henga
Naye Bi. Martina Kabisama ameongeza kuwa kutokana na wao kupewa fursa ya kutengeneza baraza la haki za binadamu nirahisi kukaa na kujadili nini tunataka kiwepo au kushugulikiwe vipi, ila upande wa wananchi itakuwa ngumu sana
Kituo cha Sheria na haki za binadamu kinakemea kitendo cha baadhi ya watu kuwekea mkazo masuala ya kisiasa pekee na kuacha mambo mengine ya msingi, Bi Anna anafunguka zaidi.

“Mpaka sasa watu wanaochambua rasimu hii wanalenga tu maswala ya siasa na kuacha mambo ya kijamii ambayo yanawalenga zaidi watanzania, hatuguswi na siasa tuu tujadili na mapendekezo ya Elimu, Afyana na mengine kama Afya ya watoto, tujadili na hayo pia sio siasa tuu” alisema Anna Henga

Asasi mbalimbali za kiraia zikiwemo LHRC na SAHRINGO hivi sasa zipo katika hatua ya kuunda mabaraza ya katiba yatakayojadili rasimu hii, kabla ya bunge la katiba litakalopitisha rasimu ya mwisho, kuundwa Mwezi Agosti mwaka huu.



EmoticonEmoticon