MAMLAKA YA ELIMU YAGAWA MADAWATI 420 KWA WILAYA YA MASASI - MTWARA




Mamlaka ya Elimu nchini imetoa jumla ya madawati 420 kwa shule za msingi 12 katika wilaya ya masasi mkoani Mtwara yenye jumla ya shilingi Millioni 79 nakuweza kupunguza upungufu wa madawati katika wilaya hiyo

Akiongea na Blog hii katika ofisi za mamlaka hiyo hii leo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkurugenzi wa TEA bi. Sylvia Lupembe amesema madawati hayo yamepunguza upungufu kutoka asilimia 22 hapo awali mpaka kufikia asilimia 17 hivi sasa

“Wilaya yote ya Masasi ilikuwa na upungufu mkubwa wa madawati lakini kwakuanzia tumeanza na idadi ya madawati 420, na hii ni awamu ya kwanza tunategemea kupeleka awamu ya pili hukohuko Masasi” alisema Lepembe

Aidha bi Sylvia Lupembe amewaomba wafadhili mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kusaidia mamlaka hiyo katika mambo mbalimbali kama ujenzi wa Madarasa, vitabu pamoja na madawati ili kuweza kuinua sekta ya Elimu nchini

“Tuchangie elimu yetu kupitia mfuko wa Elimu ili kuweza kuboresha miradi ya elimu hapa nchini, na tunapokea hata kwa wafadhili wa nje pia wandani na kushirikiana nao vyema,”Alisema Lupembe

Mkoa wa mtwara ambako wilaya ya masasi unapatikana ni miongoni mwa mikoa inayofanya vibaya katika matokea ya kidato cha nne na shule za msingi kutokana na ukosefu wa vitendea kazi kwa walimu, madarasa vitabu hata madawati.


EmoticonEmoticon