WAZIRI WA HABARI AWAKANA WANAHABARI,WAPONDWA NA WABUNGE NA HOJA YA MAUAJI YA MWANGOSI YA ZIMWA

Waziri wa Habari Mhe. Fenera Mkandara


 Hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya habari, vijana tamaduni na michezo imeendelea kujadiliwa Bungenu huku Wabunge wengi wakiwaponda wana habari kwa kukiuka kanuni za taaluma huku wachache wakitetea wana taaluma hiyo kwa kuachwa bila kujadiliwa kwa matatizo yanayo wakabili






Wizara ya habari imeomba kiasi cha shilingi Billioni 20 na ushee ili kuweza kutimiza mambo mbalimbali katika wizara hiyo, ambayo iko chini ya Waziri Fenela Mkandara ambaye hii leo amesifiwa kwa staili ya ya nywele

Katika hotuba hiyo waziri hakuweza kuzungumzia hali ya usalama ya wana habari wana mateso na mauaji ambayo yamewakumba wanahabari kama kifo cha David Mwangozi, Absolom Kibanda na hata kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi ambalo mpaka sasa aijulikani itafunguliwa lini

Hali hiyo ili mshangaza Mbunge wa viti maalum kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na maendeleo Bi. Rebeka Mgodo ambaye alishangazwa na hotuba ya Mhe. Fenera Mkandara kwa kuwasahau waandishi wa habari pamoja na matatizo yao ambayo yako wazi kwa jamii yote

“Nashangaa kutoona hata sehemu moja katika hii hotuba  ya waziri wa Habari juu ya mazingira magumu yanayo wakabili waandishi wa habari, wala mauaji ya David Mwangosi aliye uwawa na polisi huko Iringa”Alisema Rebeka Mgodo

Aidha, Bi Rebeka amewataka viongozi kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari pindi wanapofuata au kuitaji ufafanuzi wowote kutoka kwao ili kuweza kurahisisha ufanyaji kazi wa waandishi wa habari. Alisema Rebeka

Naye Mhe. John Mnyika pamoja na kupanga hoja yake kwa point nyingi wakati akiomba hoja yake kuungwa mkono na Bunge ili waweze kujadili swala la mauaji ya David Mwangosi 


Mnyika aliitaka Bunge kutengua kanuni ya 64 – 1c inayo zungumzia mbunge kuto zungumzia swala linalo subiri maamuzi ya chombo kungine hasa mahakamani, ambapo John Mnyika litaka wabunge wamuunge mkono ili waweze kuchangia na kutekeleza Ripoti ya kituo cha sheria na haki za binadamu nchini LHRC iliyoongelea juu ya mauaji ya David Mwangosi ambaye aliuwawa na askari polisi September 2 mwaka jana huko mkoani Iringa

Kabla wabunge hawaja simama kuunga mkono hoja, Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda aliingilia na kupinga hoja hiyo ambayo ilizimwa zyyy kama Analogia ndani ya Bunge hilo

REJEA HAPO JANA

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda aliunga mkono hoja Mhe.Godfrey Zambi ambaye alitaka Spika kukataa kusomwa kwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani ambayo ili wasilishwa na Mbunge wa Mbeya mjini Mhe. Joseph Mbilinyi ambayo ni bajeti kivuli ya Wazara habari.


EmoticonEmoticon