ASILIMIA 43 WAFAULU, ZIRO ZAPUNGUA MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE 2012

Matokeo mapya yaliyo subiriwa kwa hamu sana hatimaye yametoka hii leo, huku kiwango cha waliofaulu kikiongezeka na kuwa asilimia 43 hivi sasa kutoka asilimia 9.55 kwa yale matokeo ya kwanza yaliyo tangazwa tarehe 18 februari mwaka huu.

Jumla ya watahiniwa Laki 397, 138 wamefaulu, wasichana wakiwa ni Elfu 60,751 na wavulana wakiwa ni Elfu 98,858 ikiwa ni jumla ya watahiniwa wa shule Laki 159,609.

Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa, inaonyesha kuwa jumla ya watahiniwa Elfu 35,349 wamefaulu katika daraja I – III ambapo kati yao wasichana ni Elfu 10,924 na wavulana ni Elfu 24,425 ambao hawa ndio wataweza kujiunga na kidato cha sita mwaka huu kutoka idadi ya wanafunzi Elfu 35,349 ambao walifaulu hapo awali na kuacha idadi kubwa ya wanafunzi

Waliofaulu kwa daraja la IV ni wavulana ni Elfu 74,433, wasichana ni Elfu 49,827 ambao kwa ujumla wanafikia Laki 124,260 sawa na asilimia 33.54, Walipata sifuri kwa sasa ni Laki 210,846 sawa na asilimia 56.92. Matokeo ya wali jumla ya wanafunzi Laki 210, 846 walipata sifuri ambao ni sawa na silimia 56.92

Akitangaza matokeo hayo hii leo jijini Dar es salaam, Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Mhe. Shukuru kawambwa amesema maandalizi ya matokeo yaliyo tangazwa sasa yamechakatwa kwa utaratibu wa Fixed Grade Ranges lakini yakafanyiwa standalization.

“Matokeo yaliyofutwa yalikuwa yamechakatwa kwa kutumia utaratibu wa fixed grade ranges utaratibu uliotumika kwa matokeo haya mapya lakini kwa hawamu hii tumefanya standalization ilikuweza kupata matokeo haya kama ambavyo tume maalum ilivyo pendekeza” alisema

Dr, Kawambwa alielezea Fixed Grade Ranges kuwa hutumia viwango vya aina moja kuchakata matokeo kwa masomo yote bila kujali kiwango cha kufaulu kwa somo husika, viwango hivyo hubadilika kila mwaka kulingana na ufaulu wa watahiniwa kwa kila somo husika

Aidha, katika mfumo wa Fixed Grade Ranges viwango vya aina moja hutumika kuchakata matokeo kwa masomo yote bila kujali kiwango cha ufaulu kwa somo husika. Viwango vya kuchakata matokeo hutumika hivyo hivyo kila mwaka bila mabadiliko . Alisema Dr. Kawambwa

kuanzia sasa na kuendelea baraza la mitihani litaandaa matokeo ya kidato cha nne na sita kwa kutumia mfumo wa fixed grade ranges na standardisation. Alisema waziri


KUANGALIA MATOKEO MAPYA KIDATO CHA NNE INGIA HAPA




EmoticonEmoticon