JUKWAA LA KATIBA LASUBIRI HAKI MAHAKAMANI, WATAKA MCHAKATO WA KATIBA USIMAMISHWE. NCHIMBI NAYE APEWA KIBARUA KIZITO


Jukwaa la Katiba Tanzania limeamua kwenda mahakamani kupinga mwenendo wa uundwaji wa katiba mpya kwa madai kuwa mchakato unaotumika siyo wa kidemokrasia.

Akiongea na Wana habari leo Jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bw. Deus Kibamba amesema kuwa, Tume ya katiba inapeleka mchakato kwa haraka hivyo kuwanyima fursa wananchi kutoa maoni yao na kwamba wanaiomba mahakama  kusitisha zoezi la kukusanya maoni.

 “Tumeamua kwenda mahakamani kutafuta haki ya watanzania, kwani tumejaribu kufanya kila jitihada na kutoa matamko lakini hayakuzaa matunda hivyo Mahakama itatusaidia kuleta haki” Amesema Kibamba

Kibamba amesema, Tumejaribu kutoa tarifa kwa ngazi za Kibunge kwa kuonana na spika, kuonana na waziri wa sheria na katiba pamoja na kujaribu kwa ngazi za juu kwa kuomba kukutana na rais lakini haya yote hayaja zaa matunda hivyo tunaenda mahakani ambako haki ya watanzania inapatikana huko.

Bwana Kibamba aliendelea kusema, Tume ya katiba imeshindwa kutekeleza misingi 5 ya uundwaji wa katiba hivyo kuwanyima wananchi fursa ya kuleta mabadiliko kikatiba.

“Mwenendo wa mchakato wa katiba mpya hauto zaa katiba mpya Tanzania, nasema hivi kwakuwa wananchi hawajui kitu kabisa mchakato unaharakishwa bila hamasa yoyote hii haraka niyanini.” Alisema

Alitaja misingi hiyo 5 kuwa ni, Ushirikishwaji wawana siasa, kutokuwepo kwa mahakama ya kikatiba nchini kiasi kwamba wanalazimika kwenda mahaka zilizopo kufikisha madai yao. Tayari jukwaa hilo limeandaa mawakili 10 kusimamia kesi hiyo wakiongozwa na Rugemeleza Nshulla.

Aidha Bwana Kibamba ameongeza kuwa, Mchakato wa katiba mpya si vyema kuendeshwa kisiasa hivyo Wabunge wasihusishwe katika mchakato huo na kuwa wananchi wapewe nafasi kubwa ya kutoa maoni yao ili kuepusha msukumo wa chama kimoja.

Katika hatua nyingine Jukwaa la katiba limeitaka Tume ya katiba kueleza wananchi ni lini watatoa rasimu ya katiba kwani muda waliotoa tayari umepita na kwamba Mabilioni wanayotengewa na serikali yanaenda wapi.

Wakati huohuo, Jukwaa la katiba limemtakaWaziri wa Mambo ya ndani Dr. Emanuel Nchimbi asikiuke katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 19, kwani wizara yake imepanga kukiuka ibara hiyo,

Dr. Nchimbi akisoma bajeti ya wizara yake mapema Bungeni amesema serikali inapanga kupeleka muswada Bungeni wakuzuia mihadhara na maandamano yote nchini kwani wanaofanya hivyo wanasababisha uvunjifu wa amani

“Kuzuia mihadhara ndio itakuwa kama kuchohea kwani kila mtu anahaki ya kusema na kutoa maoni yake” alisema Kibamba.


EmoticonEmoticon