MASHINE ZA KUKATIA RISISTI ZITAKAZO TUMIWA NA WAFANYABIASHARA HIZI HAPA

Mashine za kukatia risiti zilizo zinduliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA wiki hii, ambazo zitatumiwa na wafanya biashara wenye kuingiza kipato cha Shilingi Billioni 14 kwa mwaka ikiwa na lengo la kuongeza kipato na kutunza kumbukumbu.

Kwenye uzinduzi huo TRA ilisisitiza sana juu ya wanunuaji kujenga tabia ya kudai risisti pindi wanapo nunua bidhaa yoyote ili kuweza kutimiza lengo la kukusanya kodi kisha kuweza kuboresha shuguli za kijamii

Mashine hizo zinapatikana kwa bei ya shilingi laki 8, natayari makampuni mbalimbali yapatayo 11 yamekuwa wakala wa TRA wa kusambaza mashine hizo kwa nchi nzima

Mashine hizo zinauwezo wa kutumia lugha ya kiingereza na kiswahili kulingana na uhitaji wa mfanya biashara au mteja, Pia itawasaidia wafanya biashara kuwa na rekodi ya mauzo ya bidhaa zake hivyo kuepuka hasara.


Adha TRA itaweza kutuma ujumbe wa maneno kupitia risisti zitakazo katwa kwenda kwa mtumiaji au kutuma taarifa ya maelezo yoyote kwa mfanya biashara, ambapo hali hiyo itarahisisha mawasiliano kati ya TRA mnunuzi na mfanya biashara


EmoticonEmoticon