ASIYE TOA RISITI KUTOZWA MILLIONI 3




Wafanyabiashara ambao hawatatoa risiti pindi wauzapo bidhaa zao watatozwa faini ya shilingi Millioni 3, ikiwa pamoja na wale watakao nunua bidhaa bila kudai risiti kutozwa Milioni 1 kwa kosa hilo





Hayo yamesemwa na Bi. Alvera K. Ndabagaye ambaye ni Afisa Elimu mwandamizi wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) alipokuwa akitoa mafunzo kwa wafanya biashara wa vifaa vya ujenzi na vipuri vya magari katika manispaa ya Kinondoni ya jinsi ya kutumia kifaa kipya cha kielctronic kwaajili ya kukatia risiti

“ Nihaki ya kisheria kudai risiti, pia nikosa kisheria kutotoa risiti baada ya kuuza bidhaa, faini kwa asiye toa ni Millioni 3 na kwa yule asiye dai ni Millioni 1” alisema Bi. Alvera

Aidha Bi. Alivera amewataka Watanzania kutambua kwamba utozwaji wa kodi ndio pato la taifa hivyo kuwa mstari wa mbele kudhibiti upotevu wa kodi, nakuacha kulalamika pale ambapo wanakosa huduma za jamii kwani kodi ndio hukamilisha hayo yote

“Tunalalamika serikali isipo kamilisha huduma za kijamii lakini hatujui kuwa kodi zetu ndio hufanya haya yote.. tuwe wazalendo tuzuie mianya ya kupotea kwa kodi ilikuleta maendeleo”

Kwamuda sasa TRA ikokwenye zoezi la kutoa Elimu kwa wafanyabiashara wa ngazi mbalimbali nchini ya jinsi ya kutumia mashine ya kielectroniki kwaajili ya kutolea risiti wakati wa mauzo ya bidhaa zao

Hatahivyo kifaa hicho hakitakuwa na ongezeko la kodi iliyopo sasa bali itashugulikia utoaji wa risiti tu. 


EmoticonEmoticon