VIJANA LAKI 7 NA 60 ELFU HAWANA AJIRA, NEEC WAJIKITA KUTAFUTA MBINU MPYA

Kutokana na swala la ukosefu wa Ajira nchini, Baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi NEEC limeamua kuwapa elimu ya kujiajiri vijana 40 ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu ili kuendeleza biashara zao na kuajiri wengine.

Akiongea hii leo katika kituo cha Ujasiriamali cha chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM, Katibu mtendaji wa Baraza hilo bwana Anecleti Kashuliza amesema wameamua kutoa elimu hiyo ili kuweza kutoa ajira kwa kundi kubwa la vijana kwa lengo la kupata ajira na kisha kuajiri wengine

Njia ya kukabiliana na tatizo la ajira nikuwapa elimu ya mitaji pamoja na kuenedeleza biashara zao, ambapo vijana 40 tuliowapata baada ya mchujo watasaidiwa kukuza biashara zao” Alisema


Vijana wengi wa kitanzania hawana ujuzi wa biashara wa vitendo, kwani wamezoeya njia ya nadharia zaidi kuliko vitendo hivyo kushindwa kujiajiri hata pindi wanapo hitimu masomo yao. Alisema Bwana Kashuliza


Hatapindi vijana wanapo jaribu kujiajiri, ukosefu wa kuendeleza mitaji huwaangusha, pia ujuzi wa kinachohitajika sokoni pia nimdogo


Uwezo wa biashara ya kushirikiana (Net-Working) inawashinda vijana waliohitimu vyuoni kuweza kufanikisha kujiajiri wenyewe, hivyo tutawawezesha vijana hawa kujiajiri ikiwa pamoja na kukuza mitaji yao iliwaweze kuajiri na wengine” Alisema


zaidi ya vijana Laki 8 ambao huingia katika soko la ajira kila mwaka nchini, laki wakiwa ni wahitimu wa vyuo vikuu, vijana Elfu 4 tu kati yao ndio huajiriwa kila mwaka hapa nchini, hii umaanisha kwamba idadi ya vijana Laki 7 na 60 Elfu hujikuta bila ajira.


EmoticonEmoticon