SERIKALI YA KIRI, UHABA WA VIFAA VYA MATIBABU NI TATIZO

Serikali imekiri kuwa uhaba wa vifaa vya tiba ni tatizo hasa kwa hospitali kubwa hapa nchini, hali ambayo ilipelekea madaktari kufanya mgomo katika siku za nyuma

Akiongea leo Bungeni katika kipindi cha maswali na majibu, Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii Mhe. Seif Rashid amekiri kuwepo kwa tatizo hilo lipokuwa akijibu swali la Mhe. Magdalena Sakaya ambaye alitaka kujua nilini serikali itatatua tatizo la uhaba wa vifaa katika Hosptali za hapa nchini ili kukomesha mgomo wa madaktari usijirudie tena.

***********

Serikali imepiga marufuku biashara za vioski ambavyo viko kwenye makazi ya watu pamoja na vile ambavyo hufanya biashara hiyo maeneo ya shule kuacha mara moja kwani vioski vingi kufanya biashara bila ya kuzingatia sheria.

Hayo yamesemwa na waziri wa Tamisemi Mhe. Agrey Mwanry alipokuwa akijibu swali la Mhe Suzan Lymo ambaye alitaka ufafanuzi juu ya biashara zinazo endelea mashuleni.


EmoticonEmoticon