MTWARA WAUKANA UZALENDO, MTU MMOJA AUWAWA, GARI YA JWTZ NAYO YAPATA AJALI




Vurugu kati ya Jeshi la Polisi na baadhi ya wakazi wa Mtwara zinaendelea hivi sasa, ambapo Mahakama, Kituo cha Jeshi la Polisi na Taraja pamoja na nyumba ya Mbunge vimeharibiwa kutokana na maandamano vurugu hizo, maeneo yaliyo adhirika zaidi ni Mtwara mjini na Mkindani

Maandamano hayo yametokana na kupinga Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ambayo imewasilishwa hii leo Bungeni

Habari zilizo ifikia Blog hii zinasema kuwa mpaka sasa, Maafa yanaendelea katika mkoa huo huku mabomu na risasi zikirindima kila kona watu wakikimbia hovyo huku polisi nao wakijitahidi kutuliza gasia hizo

Daraja la mkindani limevunjwa, mahakama ya mwanzo ya Mitenga imechomwa moto, kituo cha polisi, pamoja na maeneo ambapo kuna makapuni ya kuchimba gesi navyo vimechomwa moto.

Tayari mtu mmoja amekufa, huku wengine wakihofiwa kufa kutokana na ali hiyo. Nyumba ya Mbunge na ya mtangazaji wa TBC nayo imechomwa moto katika vurugu hizo

Habari zaidi zinasema kuwa Gari ya JWTZ nalo imepata ajali ikiwa njiani kuelekea Mwara ikitokea Nachingwea, na msaada wa kitabibu unahitajika kwa Askari hao

Hatahivyo, Waziri wa nishati namadini Mhe. Sospetre Muhongo amesema serikali imeendelea kutoa elimu kwa wakazi wa Lindi na Mtwara kujua faida ya jinsi watakavyo faidika na Gesi hiyo pia ameeleza kuwa wakazi wa mtwara waachane na fujo na maandamano kwani sio njia sahihi ya kutatua mgogoro huo

Naye Waziri wa madini kivuli ambaye Mwakilishi wa kambi ya Upinzani Mhe. John Mnyika ameitaka serikali kuweka wazi mikataba yote ya madini ilikuondoa migogoro miongoni mwa wananchi 


EmoticonEmoticon