TBS YAJA NA VIWANGO VIPYA KUDHIBITI VIWANDA, MAKAMPUNI KUTUNZA MAZINGIRA



Tanzania imeanza kutekeleza kiwango cha kimataifa cha uzalishaji kitakacho tekelezwa na viwanda pamoja na makampuni mbalimbali nchini kwa lengo la kunufaisha jamii

Kiwango hicho kilicho tolewa na shirika la viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Shirika la viwango la kimataifa (ISO) linalenga makampuni kuzalisha bidhaa kulingana na kiwango cha jamii inayo izunguka na bila kuadhiri mazigira

Akiongea na Waaandishi wa Habari hii leo katika uzindushi wa kiwango hicho mapema leo jijini Dar es salaa, Mkurugenzi wa TBS bwana Leandri S. Kinabo amesema kiwango hicho kitatumika na nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na Tanzania ndio walipewa nafasi ya kuandaa kiwango hicho

“Kiwango kimezinduliwa Tanzania lakini kitatumika na nchi zote za Ukanda wa Afrika mashariki kwa maana Kenya, Uganda watatumia kiwango hichi” Alisema Bwana Kinabo

Kinabo aliongeza kuwa, Lengo la kiwango hicho nikuzitaka kampuni na viwanda vinavyo zalisha bidhaa katika ukanda huu kuzalisha bidhaa zao huku zilikila mazingira na rasilimali watu katika maeneo yanayo wazunguka hatimaye kunufaisha jamii hiyo

“Makampuni yatatakiwa kutosababisha maafa, kulinda mazingira, rasilimali watu pamoja na njia ambazo zitaleta maendeleo katika eneo husika kama barabar”alisema

Naye mwakilishi wa Katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara ambaye ni bwana Odilo Majengo amesema kuwa kiwango hicho kinajulikana kama TZS 1323 ndicho kitatumika kwa makampuni yote ukanda wa Afrika Mahsriki kwa ajili ya viwanda na makampuni.


EmoticonEmoticon