MIAKA 150 YA READ CROSS - JAMII YAHIMIZWA KUCHANGIA DAMU




Wananchi wametakiwa kutoa ushahidi kwa wale wanao wauzia damu ilikuweza kusaidia katika kudhibiti tatizo hilo

Akiongea na Blog hii, Muhamasishaji jamii upatikanaji wa damu salama Bi. Hadija Juma kutoka shirika la Msalaba Mwekundu (READ CROSS) amesema watu wengi hutoa malalamiko juu ya kuuziwa damu lakini hawako tayari kutoa ushahidi juu ya madai yao ilikuwezesha kudhibiti tatizo hilo


Wafanyakazi wa Read Cross wakitoa huduma ya kwanza kwa msichana aliye poteza fahamu muda mfupi baada ya kutoa damu 

Hali hiyo aina madhara kiafya kwa mujibu wa Bi. Hadija Juma



“ Changamoto kubwa kwetu ni swala la kuuzwa kwa damu, watu wengi wanalalamika lakini tunapo jaribu kufanya utafiti hawako tayari kusema zaidi hivyo tunashindwa kudhibitisha, hali ambayo inapelekea kudhibiti uuzwaji damu kuwa mgumu” Alisema

Aidha, amewahasa wanawake kwa wanaume kujitolea kila mara katika kuchangia damu, kwani uhitaji wa damu ni mkubwa katika jamii. Alisema kwa wanaume unafaa kutoa Damu mara 4 kwa mwaka ambayo nikila baada ya miezi 3 huku kwa wanawake ni mara tatu kwamwaka ambayo ni kila baada ya mwiezi mi nne

“Kidaktari Wanaume inatakiwa kuchangia damu mara 4 kwa mwaka, huku wanawake ni mara 3 kwa mwaka” alisema


Naye Katibu wa shirika hilo Bi. Grace Mtui Mawalla amesema kuwa shirika hilo lina hadhimisha miaka 150 tangu kuanza kwa huduma zake za uokoaji kwa jamii Duniani, ambapo kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika mkaoni Arusha

“Maandhimisho haya yanafanyika Duniani kote, kitaifa yanafanyika mkoani Arusha ambapo mgeni rasmi atakuwani mkuu wa mkoa huo Bwana. Magesa Murongo, kauli mbiu yeti ni Miaka 150 ya huduma za kibinadamu” Alisema


Jumla ya Vijana 289 wa shirika la msalaba mwekundu wamejitokeza kuchangia damu katika makao makuu ya shirika hilo, kati ya hao vijana 61 ndio wametoa damu, 27 wameshindwa kutokana na matatizo ya kiafya ikiwemo Presha, huku wengine wakishindwa kutokana na mambo mbalimbali

Siku hiyo ya maadhimisho ndiyo siku ambayo muasisi wa shirika hilo Henry Dunant Gustave Maynier alizaliwa mnamo 8/5/1828 huko Geneva – Uswiss, ambayo nisiku ya Read Cross Duniani.


EmoticonEmoticon