WATANZANIA WAHAMASIHWA KUCHANGIA ELIMU, UJENZI WA MABWENI 30 KWA SHULE ELFU 1500

http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2013/07/TEA.jpg
  
Wanafunzi wanaoishi katika Geto au nyumba za kupanga hawapati nafasi ya kusoma kutokana na mazingira ambayo wanakumbana nayo katika nyumba hizo hali ambayo inapelekea wanafunzi wengi kufeli, kubeba mimba au kuacha shule.

Hayo yamesemwa na kaimu mkurugenzi wa ukuzaji rasilimali wa taasisi ya elimu TEA Bi Sylivia Lupembe wakati akipokea msaada wa shilingi Millioni 5 kutoka kwa kampuni ya mafuta ya GAPCO.

“Tumetembea seemu tofauti tofauti hapa nchini tumeona, mazingira nimagumu kwani mwanafunzi analazimika kupika, kuchota maji na wakati mwingine hakuna hata umeme wakujisomea, maitaji nayo yanakuwa shida kuyapata kiasi kwamba mwanafunzi anachoka na kuacha shule” Alisema Sylvia

Bi.Sylvia liongeza kuwa asilimia kubwa ya wanafunzi wanao ishi katika nyumba hizo ni wale wanaotoka katika familia duni, kwani kwa mwaka jana wanafunzi elfu 16 waliacha shule kwa matatizo mbalimbali kama ujauzito na umbali mrefu.

Mchango ulipokelewa leo na mamlaka hiyo utaelekezwa katika ujenzi wa mabweni 30 katika shule 1500 hapa nchini ili kuweza kuwawezesha watoto wakike kupata elimu bila vikwazo, kwani tayari wameanza na ujenzi wa bweni katika shule ya kibaigwa. 

Mamlaka ya elimu pia imewataka watanzania kuwekeza katika usafiri kwa wanafunzi ikiwa ninjia moja wapo ya kuchangia katika swala la kuendeleza elimu hapa nchini.
                                   ********************************

MKUTANO WA 31 WA SHIRIKISHO LA MABARAZA YA UPIMAJI NA TATHMINI YA ELIMU AFRIKA KUFANYIKA ARUSHA AUG. 12-16 MWAKA HUU

Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano wa shirikisho la mabaraza ya upimaji na tathmini ya Elimu Barani Afrika, kwa lengo la kujadili kuwepo kwa elimu ya uvumbuzi pamoja na kuinua kiwango cha walimu barani Afrika.

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini dar es salaam, Naibu Katibu Mtendaji wa baraza la Mitihani nchini Tanzania Dkt. Charles E Msonde amesema mkutano huo utafunguliwa na makamu wa pili wa Rais wa zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi huko mkoani Arusha

Mkutano huo utafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 16 Augost mwaka huu ambapo washiriki zaidi ya 400 watahudhuria mkutano huo kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda, Asia na marekani.


EmoticonEmoticon