MALERIA IMEPUNGUA KUTOKA ASILIMIA 18 MPAKA ASILIMIA 10 HIVI SASA : WAZIRI WA AFYA ASEMA



Hali ya maambukizi ya ugonjwa wa malaria nchini imepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2007 hadi mwaka 2008 mpaka kufikia asilimia 10 kwa mwaka 2012 na 2013.

Takwimu hizo zimetolewa hii leo Jijini Dare es salaam wakati wa makabidhiano ya dawa za malaria zenye thamani ya shilingi Bilion 2 kutoka China,



Waziri wa Afya na ustawi wa jamii Dr Hussein Mwinyi amewataka wazazi kuhakikisha familia nzima inatumia vyandarua vilivyowekwa dawa ili kupambana na ugonjwa huo, hayo ameyasema wakati akipokea msaada huo


Pia amewataka watanzania kufuata maelekezo wanayopewa na wataalam wa afya na kuongeza kuwa hali ya upatikanaji wa dawa za Malaria nchini ni nzuri lakini changamoto ipo katika suala la usambazaji kwenye zahanati zilizo katika maeneo yasiyofikika hasa vijijini

Hatahivyo serikali ya china imeendelea kuisaidia tanzania kwa dawa za maleria tangu mwaka 1968 ikiwa ni miaka 45 sasa, pia Waziri ameishukuru serikali ya china kwa ushirikiano wao ambao unachangia kwa kiasi kikubwa katika kutokomeza ugonjwa huo


EmoticonEmoticon