WAHAMIAJI HARAMU WATAKIWA KUONDOKA NCHINI, WANAO WALINDA KUKIONA

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi Tanzania imetangaza kuanza rasmi kwa zoezi la kuwaondoa wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakiingia na kuishi nchini kinyume cha sheria.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Dkt Emmanuel Nchimbi wakati akiongea na waandishi wa habari, ambapo Waziri huyo amesema kutekelezwa kwa zoezi hilo kunatokana na maelekezo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

“Rais tayari amekamilisha kazi yake imebaki ya waziri wa mambo ya ndani, hivyo na mimi nasema kuwa nitaanza kazi yangu ila sitawapa taarifa nilini kikubwa nikuwa watoke hapa nchini kwetu na wasivunje sheria” alisema Nchimbi

Aidha waziri huyo hakuweza kutaja muda rasmi wa kuanza utekelezwaji wa zoezi hilo na kufafanua kuwa litakuwa zoezi la kushtukiza ambapo amewataka wahamiaji wote haramu waliopo nchini kuanza kurudi kwao haraka iwezekanavyo kabla ya kuanza kwa zoezi hilo.

Jeshi la taifa, usalama wa taifa wanasubiri kauli ya kuanza kwa zoezi hilo ambalo tutalitekeleza kwa kasi ya hajabu, nakuongeza kuwa viongozi wa kijiji nao wasiwaruhusu au kuwaficha wasio watanzania hapa nchi. Amesema Nchimbi

NHC KUJENGA MAJENGO 3 DAR, YAGARIMU BILIONI 123 AJIRA ELFU 3 KUPATIKANA

Watanzania wametakiwa kutumia ardhi kwa ajili ya makazi bila kusahau suala la maeneo ya mashamba ya kilimo ili kuendeleza uchumi pamoja na upatikanaji wa chakula hapa nchini.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mh. GoodLuck Ole Medeye, wakati wa makabidhiano ya mradi wa ujenzi wa majengo ya biashara na makazi jijini hapa

Katika makabidhiano hayo Naibu waziri amesema iwapo wakandarasi waliokabidhiwa tender hiyo watachelewa gharama zitaongezeka hivyo itawalazimu kutumia pesa zao wenyewe na amewataka kukamilisha kazi kwa wakati.

Zaidi ya shilingi bilioni 123 zitatumika katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi na biashara jijini Dar es Salaam katika mradi unaoendeshwa na shirika la nyumba la taifa, mradi ambao utakamilika baada ya miaka miwili na nusu ikiwa na lengo la kuweka makazi ya kisasa.

Mradi huo pia utaweza kuajiri watanzania zaidi ya Elfu 3 na kuongeza majengo ya kibiashara pamoja na nyumba zaidi ya 520, Mkurugenzi wa ubunifu wa shirika la nyumba la Taifa NHC amesema majengo hayo yatajengwa katika maeneo ya Kinondoni- Hananasif, Upanga na Victoria jijin Dar es salaam.

Miradi hiyo mitatu ya nyumba za makazi na majengo ya biashara imegawanywa katika muda tofauti mpaka kukamilika kwake, mkubwa zaidi utachukua miezi 30 kukamilika na mdogo utachukua miezi 18 kukamilika na nyumba hizi zitauzwa kwa watanzania.

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi Tanzania imetangaza kuanza rasmi kwa zoezi la kuwaondoa wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakiingia na kuishi nchini kinyume cha sheria.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Dkt Emmanuel Nchimbi wakati akiongea na waandishi wa habari, ambapo Waziri huyo amesema kutekelezwa kwa zoezi hilo kunatokana na maelekezo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

“Rais tayari amekamilisha kazi yake imebaki ya waziri wa mambo ya ndani, hivyo na mimi nasema kuwa nitaanza kazi yangu ila sitawapa taarifa nilini kikubwa nikuwa watoke hapa nchini kwetu na wasivunje sheria” alisema Nchimbi

Aidha waziri huyo hakuweza kutaja muda rasmi wa kuanza utekelezwaji wa zoezi hilo na kufafanua kuwa litakuwa zoezi la kushtukiza ambapo amewataka wahamiaji wote haramu waliopo nchini kuanza kurudi kwao haraka iwezekanavyo kabla ya kuanza kwa zoezi hilo.


EmoticonEmoticon