Mufti Mkuu awataka waislamu kuchangia Damu siku ya Maulid


Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametangaza siku kuu ya kuzaliwa Mtume Muhamad ya Maulid maarufu kwa jina la Maulid Day, kitaifa itasomwa siku usiku wa tarehe 11 mwezi wa 12 mwaka 2016 katika Mkoa wa Singida Wilaya ya Iramba.

Akiongea na vyombo vya habari jijini Dar es salaam, Mufti Mkuu Sheikh Abubakar Zubeir amesema Maulid ya mwaka huu yataadhimishwa kwa namna tofauti ambapo waumini wa kiislamu kote nchini watatakiwa kuchangia damu na kufanya zoezi la usafi katika maeneo yao mara tu baada ya ibada.

Kipenzi chetu Bwana Mtume Muhammad amesema “Uislamu ni Usafi basi jisafisheni kwani hakika hataingia peponi isipokuwa Msafi, mwamisingi hii mimi mwenyewe nitaongoza usafi kufurahia kuendana na kuiga na kutekeleza mafundisho yake” amesema.

Aidha, amewataka viongozi wa Baraza kusimamia na kuhimiza amani ya nchi yetu na kutokuwa tayari kuwavumilia wale wote ambao wanataka kuharibu amani na utulivu katika nchi yetu.


Kauli mbiu ya Maulid ya mwaka huu ni Muislamu jitambue badilika amani na usalama ndio maisha yetu” hivyo nijukumu la kila muumini wa dini ya kiislamu na waumini wa madheebu mengine kutunza amani. Amesema.


EmoticonEmoticon