Jumia Market kufanya punguzo la pei kwa asilimia 80 msimu wa sikukuu

Imebainishwa kuwa kufanyabiashara kwa njia ya mtandao hupunguza garama kubwa ya uendeshaji kibiashara kutokana na biashara za mitandao kuto hitaji eneo maalum la kufanyia biashara na kugarimu fedha kidogo na kuwafikia watu wengi zaidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa ukanda wa Afrika Mashariki, kutoka kampuni ya uuzaji bidhaa kwanjia ya mtanda ya JUMIA – MARKET Bwana Justine Christianson ameiambia East Africa Radio katika mahojiano maalum kuusiana na biashara kwanjia ya mtandao, na kusema kuwa kunaurahisi mkubwa kuendesha biashara mitandaoni.
Huduma za mtandao zinamrahisishia mteja kununua na kupata bidhaa kwa wakati pamoja na kuepuka kutumia gharama za ziada kama usafiri kutokana na wateja kupelekewa bidhaa majumbani mwao” amesema
Christians, amesema katika nchi za Africa Mashariki Tanzania imeonekana kukuwa kwa shuguli za kimtandao huku nchi ya Kenya ikiongoza kwakufanya manunuzi mitandaoni ambapo aliwashauri vijana kutumia muda wao kubuni njia za kujipatia kipato bila kugarimu fedha mitandaoni.
Meneja Mkuu wa JUMIA MARKET nchini Tanzania Bwana Laurite Elmshauser amesema ili kuhakikisha watanzania wengi wanatumia mitandao kununua bidhaa, kampuni yao JUMIA imefanya punguzo la bei za bidhaa zake kwa asilimi 80 katika wiki yake ya maadhimisho ya Black Friday.
Meneja Masoko wa JUMIA MARKET Bi. Herrieth ngolwa amesema kampeni hiyo ijulikanayo kama Black Friday itakuwa ya siku 5 kuanzia Tarehe 21 Nov hadi 25 Nov ili kuwawezesha watanzania kununua bidhaa za msimu wa krismas kwa punguzo la pei kwa kutembelea mtandao wa JUMIA.






EmoticonEmoticon