Asilimia 60 ya wananchi wanatamani kuamisha watoto wa kutoka shule za serikali



Asilimia 50 ya wananchi waliohojiwa katika utafiti wa kubainisha ubora wa elimu katika shule za serikali tangu kuanzishwa kwa mpango wa elimu bila malipo ya adda wamekiri elimu kuboreshwa licha ya kuwa asilimia 60 ya wananchi kutamani kuwasomesha watoto wao katika shule binafsi.

Utafiti huo pia umebainisha kuwa asilimia 34 ya wananchi wamelalamikia ukosefu wa waalimu, asilimia 30 wamelalamikia ukosefu wa madawati na asilimia 13 wakilalamikia ukosefu wa  madarasa, wengine wakilalamikia ufundishaji na ukosefu wa chakula kwa wanafunzi.

Mkurugezni mtendaji wa TWAWEZA Aidan Eyakuze amesema idadi hiyo ni ya wananchi kati ya 1,806 waliohojiwa Tanzania bara ambapo amesema asilimia 35 wamesema ubora wa elimu umemebaki palepale na wengine asilimia 15 wamesema ubora umeshuka kabisa.

Adha Tafiti hiyo pia imebaini kua asilimia 85 ya wazazi hawajiusishi na masuala ya masomo ya watoto wao, huku asilimia 83 imekuwa ni changamoto za miundombinu na matokeo mabaya ya wanafunzi na utovu wa nidhamu kwa wanafunzi


Utafiti huo umefanyika kati ya Agosti 7 na 14 mwaka huu hata hivyo baadhi ya wasomi walioshiriki uwasilishwaji wa ripoti hiyo kutoka chuo kikuu cha elimu wamesema matokeo hayo ayaendani na uhalisia wa hali ya elimu nchini na kwamba elimu aiwezi kuwanaubora kwa kipindi cha mwaka mmoja pekee.


EmoticonEmoticon