MWANAJESHI WA JWTZ ALIYE UWAWA DRC AZIKWA LEO MAKABURI YA KISUTU



Mwili wa askari aliyeuawa kwa kupigwa risasi Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC Afisa Luteni Ahmad Rajab Mlima umeagwa na kuzikwa leo katika makaburi ya kisutu jijini Dar Es Salaam.

Mwili huo uliagwa katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Lugalo ambapo heshma za kijeshi zilitolewa kisha mwili huo kupelekwa nyumbani kwao Mbezi Beach kwaajili ya kuagwa na familia kisha kupelekwa katika makaburi ya Kisutu kwa maziko.

Akisoma Risala kwa niaba ya mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania, Jenerali Davis Mwamunyange, wakati wa shughuli ya kuagwa kwa askari huyo, Mnadhimu mkuu wa jeshi Luteni Jenerali Samwel Albert Ndomba amesema, Luteni Mlima alikumbwa na umauti wakati akilinda amani katika mji wa kiwanja uliopo mpakani mwa DRC, Rwanda na Uganda.

Luteni General Samwel amesema, Marehemu alikuwa na wenzake katika shuguliza kulinda amani ndipo alipigwa risasi na watu ambao hakuwataja siku ya Jumapili tarehe 27 nakufariki hapo hapo. Alisema Luteni General Samwel

Aidha mgeni rasmi katika shughuli hiyo, Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Mh. Shamsi Vuai Nahodha amesema, pamoja na kumpoteza Luteni Ahmad, bado Jeshi la Tanzania litaendelea na Operesheni ya amani nchini DRC, nakuhakikisha kuwa amani inakuwepo nchini humo

Naye kaka wa marehemu Dr. Aziz Mlima ametoa shukrani kwa jeshi la Tanzania na jeshi kwa ujumla kwa kushiriki katika msiba wa ndugu yake.ambapo marehemu ameacha mtoto mmoja na mchumba ambaye walitarajia kufunga ndoa Dec. mwaka huu.

Huyu ni mwanajeshi wa 3 wa Tanzania kuuwawa ndani ya mwaka huu tangu Majeshi ya Tanzania kupeleka majeshi yake nchini humo.Hatahivyo mapambano yanaendelea ambapo hivi sasa majeshi ya serikali yamefanikiwa kuteka ngome ya M23 huko Goma ambapo mkuu wa jeshi la waasi amekimbiliwa nchini Uganda.


EmoticonEmoticon