SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA KODI KWA BIDHAA ZA SAMANI ZINAZO AGIZWA NJE

Serikali imeshauriwa kuongeza kodi katika bidhaa za samani zinazoingizwa hapa nchini ili kuweza kuongeza dhamani ya soko la samani zinazo tengenezwa hapa nchini na kuwawezesha wabunifu wa ndani kujiongezea kipato.

Akiongea katika mahafali ya kuhitimu kwa wanafunzi wa chuo cha ufundi cha Mtakatifu Gasper pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiy Mkuu wa chuo hicho Padri Achileus Mutalemwa amesema kuwa ni vyema serikali ikatambua kuwa samani kutoka nje ni chanaga moto kubwa kwa watanzania wao jishugulisha na fani hiyo.


“Kwa bidhaa za samani zinazo agizwa nje endapo serikali ingeoweka kodi kubwa ingewezesha wauzaji wa ndani kuwa na faida lakini kodi yao nisawa na kodi za wauzaji wa ndani jambo linalopunguza ushindani wa kibiashara na kipato” alisema Padri Mutalemwa

Baadhi ya wanafunzi ambao wanasoma masomo ya ufundi wame waasa wanafunzi wenzao kupenda masomo ya juwawezesha kujiajiri mara tu wamalizapo masomo yao pamoja na kuwa wabunifu

Wanafunzi hao ni Tumainieli Makundi ambaye alionyesha uwezo katika kutengeneza sofa, kabati na meza huku mwenzake Adson Bang akionyesha umahiri katika kutengeneza meza ambayo pia inatumika kama mbuzi ya kukunia nazi.

Shule ya mtakatifu Gasper kwa ngazi ya chuo ilianzishwa mwaka 1988 kwa lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa kuwafundisha wanafunzi jinsi ya kujitegemea, na kwa upande wa shule ya sekondari ilianzishwa mwaka 2010 ikiwa chini ya taasisi ya kidini.


EmoticonEmoticon