WANANCHI 40,000 WALIA NA TATIZO LA MAJI HUKO ARUMERU



Wananchi zaidi ya 40,000 wa vijiji 30 katika wilaya za Arumeru na Longido mkoani Arusha wanakabiliwa na tatizo kubwa la kukosekana kwa maji katika maeneo yao kutokana na uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji unaoendelea katika maeneo yao

Vyavyo vya maji vilivyo adhirika katika chemchem zinazotoka katika msitu wa mlima Meru huku serikali ikiombwa kuchukua hatua za haraka kukabiliana na tatizo hilo.

Uharibifu huo umefanyika katika kata ya ngarananyiki ambapo wananchi na viongozi wa kata hiyo wamesema pamoja na kufanya jitihada za kudhibiti tatizo hilo bado linaendelea nakuomba serikali katika ngazi za juu kuliangalia suala hilo kabla madhara hayajawa makubwa

Wananchi waliotoa ombi hilo ni pamoja na Julius Ayo, Furaha Mungure na Barnaba Simon, ambapo wamesisitiza kuwa kuharibiwa kwa vyanzo hivyo ndio chanzo cha hatari ya kukosekana kwa maji safi na salama katika maeneo yao


Aidha baadhi ya viongozi na watendaji wa ngazi mbalimbali wakiwemo wale wakutoka katika kamati ya mazingira wametembelea eneo hilo na kujionea hali halisi na kuahidi kufikisha suala hilo katika ngazi ya mkoa
Viongozi hao ni Bwana Onesmo Nangole ambaye ni mwenye kiti wa mkoa wa Arusha kwa tiketi ya chama cha CCM.


EmoticonEmoticon