HABARI GROUP YAANZISHWA KUNUFAISHA WAANDISHI WA HABARI


Waziri wa maliasili na utalii, Balozi Khamis Kagasheki amewataka waandishi waabari wa kike kutumia kalamu zao katika kuandika mambo yanayo hamasisha amani na utulivu nchini

Waziri huyo aliyasema hayo katika uzinduzi wa kikundi cha HABARI GROUP, ambacho mlezi wake ni Naibu Waziri wa katiba na sheria Mhe. Angella Kairuki ambaye aliahidi kuwa bega kwa bega na kikundi hicho ilikuhakikisha kuwa kundi hilo linasonga mbele

Kagasheki alisema, Uwezeshwaji wa wanawake kiuchumi ni moja ya maadhimisho 12 ya ulingo wa Beling hivyo mnachofanya hapa ni katika kujikwamua wenyewe kiuchumi na kama mnavyofahamu wanawake wanamajukumu mengi katika familia, tasnia pia imewabana sana ila bado mmethubutu kufanya kazi, endeleeni hivyo hivyo” Alisema

Aidha, Mratibu wa kikundi hichi Bi. Rabia Bakari amesema kuwa kikundi hicho kinahitaji zaidi ya Sh.Millioni 10 ilikuwawezesha wanachama wake kupata mikopo itakayo wanufaisha 

“Kwa sasa katika akaunti yetu tumefanikiwa kuwa na million 2 nanusu tu, hivyo tunaitaji zaidi ya Milioni 23 ilikuweza kukopeshana na kukamilisha malengo ya chama hicho” Alisema Rabia

Hatahivyo waliweka kukusanya zaidi  ya sh. Millioni 6 katika uzinduzi huo, ambapo mgeni rasmi alitoa Milioni 2.


EmoticonEmoticon