WAZIRI WA ELIMU ATAKA VETA KUUNGANA NA COSTECH


WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako amesema kwa mwaka huu wa fedha, wamejipanga kuhakikisha wanafufua karakana zilizopo na kuhakikisha zinaendana na matakwa ya serikali ya Viwanda.

Akizungumza wakati alipotembelea katika banda la VETA, Ndalichako alisema pamoja na kufufua karakana zilizopo Veta pia wataongeza wigo wa kuhakikisha zinakuwa nyingi na kuboreshwa.

Alisema kazi inayofanywa na VETA ni kubwa ila tatizo lipo kwenye kujitangaza ili kuweza kuuza bidhaa zao.
"Kazi wanayofanya Veta ni kubwa, lakini changamoto ipo kwenye kujitangaza, bado hawajajitangaza katika kutoa huduma zao. Hivyo tutashirikiana na Costech ili kuendeleza VETA na kupunguza kuagiza vitu kutoka nje ya Nchi," alisema.

Ndalichako alisema tatizo linalosababisha la Veta kuwa chache ni gharama zake kwani jengo moja linagharimu bil. 9, hivyo wameshawaagiza Veta kupitia upya gharama kwa viwango tofauti tofauti ili kupata Veta nyingi.


Aidha Ndalichako aliwapongeza Veta kwa tuzo waliyoipata na kusema kwamba walistahili kupata tuzo hiyo kutokana na ubunifu walioufanya kwa vitu mbalimbali ikiwamo pampu ya kamba, bustani ya kuhama na jiko la kukaushia mboga.


EmoticonEmoticon