MUSIC&MOVIE

Ngoma ya Feza Kessy ambaye ni mwakilishi wa Tanzania ndani ya Big Brother Africa. Fezza ameendelea kufanya vizuri katika jumba hilo na kuiweka Tanzania katika nafasi nzuri


******************************************************************
Msanii aliyejulikana kama KASHI kwajina kamili ni Jaji Hamisi ambaye amefariki jana baada ya kuugua kwa siku tatu, amezikwa katika makaburi ya Anansif Kinondoni hii leo maajira ya alasiri


Kashi ameacha watoto wawili pamoja mume, kwamujibu wa mama mzazi wa marehemu arehemu alizaliwa mwaka 1976 huko mkoani Lindi

Pichani ni Mama wa marehemu Kanumba, mama yake Lulu akiteta jambo na mama yake Monalisa




***************************************************
CD ZISIZO NA CHATA YA TRA KUPIGWA STOP JULY MOSI


Baraza la sanaa Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la hatimiliki nchini zimejipanga kuzuia mauzo ya CD za wasanii wa bongo ambazo hazina chata ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), ili kuongeza kipato cha wasanii na Taifa kwa ujumla.

Wakiongea na Blog hii leo Dar es salaam, Kaimu katibu mtendaji wa BASATA bwana Godfrey Lebejo na Mtaalamu wa Tehama kutoka COSOTA wamesema zoezi hilo litaanza rasmi July 1 mwaka huu.

Kwa muda sasa wasanii wa bongo wamekuwa wakilalamika kuibiwa kazi zao, hivyo mamlaka hizi zimeamua kutumia mbinu mpya ya kudhibiti kazi hizo kwa lengo la kuinua maslahi ya wasanii.


*******************************************************************
BAHATI BUKUKU AHAMIA KENYA, NA NGOMA YAKE MPYA - NAKUTEGEMEA

Katika hali ya kushangaza msanii nguli wa nyimbo za injili nchini Bahati Bukuku ameandika katika mtandao wa ou tube wimbo wake mpya kuwa ni muimbaji wa Kenya
                              
                                  

Ngoma hiyo mpya ambayo imesambazwa kwenye mtandao wa You Tube inamtambulisha kama mkenya Nakutegemea - Bahati Bukuku New Kenyan Gospel music 2013 ?

****************************************************************************

NGOMA KALI KUTOKA KWA DESIRE  LUZINDA, UNAITWA NSUBIZA

                   
                   MSANII WA UGANGA
*************************************************************************
SIKILIZA HAPA***HAKI YETU- NGOMA MPYA YA KIDUMU 




Mwanamuziki Jean Pierre Nimbona Alias a.k.a KIDUMU ametoa wimbo mpya unao kwenda kwajina la HAKI YETU, ambao unaongelea zaidi maswala ya haki na usalama ujumbe kwa jamii yote kujali HAKI.

Kidumu ni raia wa Burundi ambaye aliamia nchini Kenya wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994, lakini yeye aliingia nchini Kenya 1995. mwaka 2001 alitoa Album yake ya kwanza inayoitwa Yaramenje, amekuwa akiimba kwa lunga yakirundi Kiswahili na Kingereza kidogo

Kidumu ameimba nyimbo 18 zikiwemo alizo imba mwenyewe na za kushirikishwa. Wimbo huu mpya Kidum amemshirikisha Nemless

Haki yetu umeandikwa na Kelvin Swamwel, Thiorry de Oliviera na Nimbona Jean Piere aka Kidum, Ngoma imetengenezwa na Robert "rkay" Kamanzi na Steven Waweru na Producer wake ni Robert"rkay" studio ya MingiLove Studios.

Posted: April 05.2013
*********************************************************************************

MERCY JOHNSON AMUANIKA MTOTO WAKE


Msanii maarufu wa maigizo barani Afrika ambayea anatokea pande za Nigeria, bibie Mercy Johnson amemuanika mtoto wake, Mtoto huyo anaitwa Baby Purity Ozioma Okojie’s anatarajiwa kufanyiwa sherehe wiki ya kwanza ya mwezi wa tatu huko Lagos Nigeria





***************************************************************************************************************************

WIZ KHALIFA NA AMBER ROSE WAPATA MTOTO WA KIUME. 


Rapper Wiz Khalifa na Mchumba wake Amber Rose wamemkaribisha duniani mtoto wao wa kwanza leo asubuhi. Mtoto Huyo wa Kiume amepewa Jina la Sebastian Taylor Thomaz Aka "The Bash." Baada Ya Mtoto Kuzaliwa Wiz Khalifa Ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter "Daddy time," "Happy Birthday Sebastian "The Bash" Taylor Thomaz!!! ` Everyone welcome this perfect young man into the world.

 **************************************************
LINEX KUMUANIKA MCHUMBAWAKE, SIKUYAKE YAKUZALIWA HUKO ARUSHA
 
Msani Linex leo anatarajia kumuanika mpenzi wake kwenye siku yke yakuzaliwa ambayo itafanyika huko mkoani harusha, Leo katika sherehe aliyo andaa nimoja yakitu ambaho kinasubiriwa na wengi ilikumjua mridhi wa mama halima

Hatahivyo kunatetesi kuwa mrembo atakaye wekwa wazi ni mchumba wake wa kizungu ambaye amekuwa akionekana naye kwa karibu sana na ambaye amewahikukiri kutoka naye


Linex anasherekea siku yake ya kuzaliwa hii leo ikiwa alizaliwa tarehe 15. 2 lakinimiaka yake ameweka kapuni, na itafanyika huko Arachuga

Linex ambaye anafanya vizuri sana ndani ya game ya bongo fleva huku akiwa na style yake ya kuweka manjonjo ya kiluga chake kwenye nyimbo. Pia Linex Yumo ndani ya kundi la Lekalutigite ambao ni muunganikano wawasanii kutoka Kigoma


Posted on. 15.02.2013
 ***********************************************
MABAYA KUMKUTA DIAMOND,MGANGA WAKE AFUNGUKA

 Msanii maarufu nchini Diamond Plantnum ameingia katika kashfa nyingine baada ya mtu anaye dai kuwa ni mganga wake kujitokeza na kumpa makavu kwenye vyombo vya habari

Akiongea Katika kipindi kilichorushwa na kituocha TV cha EATV kipindi cha Hotmix, mganga huyo aliye julikana kwajina la Ustadhi Yahaya wa Kigogo jijini Dar es salaam, amesema jinsi anavyosikitishwa na msanii huyo kusema kuwa hajawai kwenda kwa mganga wala kufanya ushirikina waaina yoyote ilikujiinua kisanii

Mganga huyo amesema, anashangazwa na kitendo cha Diamond kusemekana kuwa ni freemason wakati yeye ndiye  aliyemuinua kisanii pka akufikia hapo 

Aidha mganga huyo alipoulizwa niya yakufanya kama anamchafulia msanii huyo, alidai kuwa yeye hana nia hiyo ila kitendo cha Diamond kujidai anampotezea na kutopokea simu yake kwa muda mrefu sasa baada ya kupata umaarufu nakung’ara kimuziki

Mganga huyo aliweza kusoma SMS ambayo alimtumia mwaka jana msanii huyo kumweleza kuwa anacho kifanya sio poa kwani yeye ndiye aliyemtoa kisanii na kuzidi kulalamika kuwa hata simu zake hapokei
Mganga huyo kudhibitisha kuwa anamfahamu zaidi Diamond alisema kuwa miaka ya nyuma kidogo aliwahi kukutana hata na mama wa msanii huyo kwani familiya zao zinafahamiana 

Hatahivyo Mganga huyo akueleza wazi kama kweli anamdai Diamond pesa yoyote ambayo anahitaji kupewa na msanii huyo, na kueleza kuwa maagano aliyoweka naye ndiyo chanzo cha kila kitu mpaka yeye kufikia hatua ya kusema habari hizo

Mganga huyo alitoa maneno ya kumlaani Msanii msanii huyo, kwakusisitiza kuwa kitakacho mtokea msanii huyo kitaonekana

Kwamuda wa mwaka hivi kumekuwa na lawama akitupiwa msanii Diamond kuwa anamtesa na kumroga msanii mwenzake ambaye alikuja kwa swaga kama zake msanii Tanzanite ambaye naye Alisha muomba msamaa msanii huyo iliasimroge na Diamond kukana matukio hayo nakusema kuwa amemsamee msanii huyo
Kama haitoshi kumekuwa na kashfa ya yakumwambia msanii huyo ni Mshiriki wa Dini ya kimashetani ya Freemason, tuhuma ambazo Diamond amezikana kuwa sio za kweli nahata Blog hii iliwahi kuandiika habari isemayo DIAMOND AUKANA U FREEMASON 

Diamond mwenyewe kupitia vyombo mbalimbali vya habari amekuwa akikana kumjua mtuhuyu ambaye anadai kuwa alikuwa ni mganga wake

Posted on: 5th Feb.2013
*********************************************************

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WASANII WA MAIGIZO 

Serikali imekubali kukaa na Wasanii wa Filamu ilikusikiliza madai yao juu ya maswala ya kanuni za Tozo zilizopendekezwa wakati wa kupitia kazi za wasanii (Filamu) kabla ya kufika Sokoni

Mike Sangu, Mwenyekiti wa Chama cha Wasanii maigizo nchini, amesema kuwa Tayari wameanza mazungumzo na Serikali juu ya kanuni hizo, iliwaweze kuangalia njia mbada ya kufanya juu ya Kanuni hizo ambazo zilikuwa zinawakandamiza sana upande wa mapato

Mike Sangu- M/Kiti wa chama cha w
“ Tayari tumeanza mazungumzo na Serikali juu ya Kanuni hizi mpya na tunaamini kuwa mambo yataenda sawa kama tunavyo tarajia, Alisema Mike

Aidha kulikuwa na mgogoro juu ya kanuni mpya katiya TAFF, COSOTA na Chama cha Waigizaji nchini, ambapo Serikali kupitia Wizara ya Habari, Tamaduni na Michezo.


Hatahivyo, Mike Sangu ameongelea hali ya Msanii mwenzao Matumaini ambaye anahali mbaya huko nchini Msumbiji alikoenda kwa shuguli za kikazi, nakuongeza kuwa Wanaomba watu wenye nianjema watoa mchango wa hali na mali ilikuweza kumasafurisha kuja Nchini kwa matibabu zaidi. Alisema Mike
Msanii wa maigizo Matumaini anaye umwa hivi sasa


Mike Saangu, ametoa nomba yake ya Simu kwaajili ya watu wanaoitaji kutoa mchango wao na kiasi kinacho hitajika ni Shilingi Milioni Moja. 1,000,000 kama nauli ya kumsafirisha msanii huyo



“ Matumaini kazimba sana miguu na hali yake nimbaya, msamaria yeyote anaweza kumchangia ni 0718951355 kwaajili ya kukata tiketi ya kumsafirisha arudi nchini” Alisema Mike

******************************************

 HUYU HAPA MTOTO WA BOB JUNIOR 
****************************************** 
  MSANII WA BONGO FLEVA ASHANGAZA MSIBANI  KWA SAJUKI

Msanii mkongwe na maarufu wa Bongo Fleva leo katika msiba wa Sajuki amekataa kuhojiwa na waandishi wa habari kwa madai ya kutotaka kuonekana kiherehere anapohuzuria misiba.

Msanii huyo ambaye jina lake nalihifadhi, alisema "Sipendi kuonekana kiherehere kwa sananii wenzangu kwani mimi naonekana sana kwenye kila msiba wa wasanii wengine"

Kituambacho nimekiona mimi nikuwa wasanii wa Bongo Fleva wanabagua wasanii wengine hasa kutokana na kitendo cha msanii nguli na mkubwa kukataa kuhojiwa juu ya msiba kwa kuhofia kuona anaki herehere miongoni mwa wasanii wengine.

Msanii huyu wa Bongo Fleva alijitokeza sana katika mazishi na msiba wa sharomilionealakini katika mazishi ya sajuki alijificha na kukataa kuhojiwa iliasijulikane kama alihudhuria mazishi ya sharo Milionea


**********************************************

.................................................................................

AKILI THE BRAIN ARUDI TENA NA NGOMA MPYA YA MY DEAR


Msanii wa bongo fleva na muandaaji wa Muziki nchini ambaye alitamba na kibao cha Regina, arudi tena

 Akili the brain, ambaye kwa muda kidogo alikuwa kimya sana baada ya kutoa ngoma ya Regina, 
hivi sasa anakujia na wimbo wa My Dear

Katika wimbo huo wenye miondoko kama ya kiindi amem..
hirikisha msanii sa-raha

Akili, amejikita zaidi kwenye uproducer licha ya kuwa na uwezo wakutunga mistari na kuimba.

     ..............................................................
RAY, WOLPER NA IRENE UWOYA WAJINYAKULIA NAFASI ZA JUU UONGOZI WA BONGO MOVIE

Vicent Kigosi maarufu kama Ray ameibuka kidedea na kuwa Mwenyekiti wa Bongo Movie, baada ya uchaguzi uliodumu kwa miezi miwili hivi sasa, na kumbwaga JB aliyekuwa Mwenyekiti katika uongozi uliopita.



katika Uchaguzi huo, Irene Uwoya aliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Mpya, huku Jackline Wolper akiibuka kuwa Makamu mtunza Fedha.




Nchiki Mchoma awa katibu Mkuu wa Bongo Movie, Uchaguzi huo ulichelewa kutokana na Tasnia ya Filamu kupatwa na Misiba mfululizo. Ambapo kwa wiki moja walimpoteza Sharo Milionea, John Steven Maganga na Mropero.
.
 .............................................................................

PRESIDENT OF CRAZY ATOA NGOMA MPYA

president of crazy- Mkono wa Mkonole, Awachana wasanii kupenda kazi za wasanii wenzao, huku akiachia ngoma kali ya Bayoyo yenye miondoko ya serious comedy.


Ukiongelea sanaa ya vichekesho nchini nilazima umtaje Mkono wa Mkonole, mabye tangu enzi za Kaole sanaa Group anakamua vizuri sana kwenye vichekesho.na hivi sasa ameibukia muziki 

Mkonole tayari ametoa ngoma mbili, iliyopo sokono kwa sasa inakwenda kwa jina la BAYOYO. ngoma ambayo inamiondoko ya serious Comedy.

Mkonole amewashukuru sana watanzania kwa kupokea kaziyake ya Bayoyo pia kwa kuendelea kuipenda kazi yake ya sanaa ya maigizo.

Amekemea kitendo cha Wasanii wenzake kutafuta mbinu za kuupotezea muziki wake ili usivume kuwa sio cha kiungwana na kuwataka kutokufanya hivyo, zaidi amewataka wasanii kupenda kazi za wenzao.
 

....................................................................................................................................

JACKLINE CLIF VIDEO QUEEN VIDEO YA  DIOMOND, NATAKA KULEWA 

Msanii wenye viwango vya juu Bongo, Nasibu Abdul a.k.a Diamond Plantum au Asali ya Warembo ametoa Video yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa muziki wake.inayokwenda kwa jinala Nataka kulewa, huku mrembo Jacquline Clif akikamua poa msana ndani ya Video hiyo


katika Video hiyo ambayo Diamond kaonyesha uwezo wa juu kwa ubunifu wake nakumtumia mrembo kadhaa kukamilisha dhana ya kuchoshwa na mapenz so anataka kulewa, na swagga za mkali wa HipHop mareemu Michael Jackson zimo ndani.

 Tayari ngoma hiyo iko kwenye mitandao na kwenye vyombo vya habari hapa nchini.

................................................................................................................ 
WASANII KUTOZWA ELFU 20 NA NSSF

Wasanii wa Filamu nchini Wamekubali kujiunga na NSSF
Wasanii wa Filamu wamekubali kujiunga na mfuko wa hifadhi wa jamii NSSF ilikuweza kuwasaidia pale wanapo kutwa na majanga mbalimbali kama msiba na majanga mengine ya kijamii,

akiongea kwa niaba ya Wasanii wenzake, Miss Tanzania wa zamani na Muingizaji wa Filamu nchi Wema Sepetu, amesema wakotayari kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ilikuweza kunufaika na mafao mbalimbali kama Fao la Mazishi na mengineyo.
Naye Msanii Maarufu Odama, alielezea furaa yake juuya uamuzi ambao NSSF umeufanya wakuweza kuwashawishi kujiunga na mifuko ya mafao kwani faida zake ninzuri na kuongeza kuwa Kiwango ambacho kitatozwa cha shilingi elfu 20,000 nichachini kiasi cha wasanii wote wenye uwezo na wasio na uwezo watamudu kutoa garama hizo.
Kwa upande wake Yusuf Mlela, alisema kuwa swala la kujiunga na mfuko wa hifadhi za jamii nimuhimu kwakila mtu na aumbagui mtu, nakuwataka wasanii wote waione fursa hio kuwa ya kipekee kwao


........................................................................................................................................................................ 

Shilole ashindwa kuimba wimbo wa kumuenzi   Sharo Milionea
                     Msanii wa Muziki na Maigizo nchini Shilole, ameshindwa kuimba wimbo uliotungwa kwaajili ya kumuenzi mareemu Sharo Milione, aliyepoteza maisha taree 26 majira ya saa 2 usiku, baada ya kufika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.
 Wasanii mbali mbali wa Bongo Fleva wametoa ngoma inayo itwa KAZAMOYO ya kumuenzi msanii mwenzao marehemu Sharo Milionea, wimbo ulioimbwa na kurekodiwa katika studio ya Kiri Records chini ya Producer C9
Miongoni mwa wasanii walioshiriki katika nyimbo hiyo, ni Shilole, Barnaba, Sheta, Richimavoko, Dayna Nyange, Suma Mnazaleti, Kanali Top na wengine wengi
Hatahivyo kundilake la zamani la Watanashati nao kwa upande wao walitoa Ngoma ya kumuenzi Mareemu Sharo Milionea

2 comments

inapendeza sana blog yako. hongera kwa kuweka habari nzuri.

Asante sana endelea kutembelea ukurasa hu


EmoticonEmoticon