WALIOGUSHI VYETI SERIKALINI SASA KUBAINIKA, UHAKIKI MPYA WA WATUMISHI HEWA



Serikali inatarajia kuendesha zoezi la uhakiki wa Watumishi wa umma kote nchini kwa siku 14 kwa kutumia mfumo wa kielektroniki ili kuondoa watumishi hewa na wenye utambulisho danganyifu.

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais menejmenti ya utumishi wa umma na utawala bora Mhe. Angela Kairuki amesema zoezi hilo litahusisha uchukuwaji wa alama za vidole, vyeti vya elimu, cheti cha kuzaliwa na hati ya malipo ya mshahara, Hati ya kusafiria, kadi ya mpiga kura na Kitambulisho cha Kazi.

Mhe. Kairuki amesema lengo nikuuimarisha mifumo ya usimamizi wa raslimaliwatu na mishahara kwakutumia kanzi data ya utambulisho wa Taifa ambapombo zoezi hilo litaendeshwa na mamlatka ya vimbulishi vya taifa na kwamba zoezi hilo litaanza Octoba 3.2016.

Tuna watumishi wa serikali Laki 5 na elfu 61 lakini uhakiki huu utatupa fursa ya kuwatambua zaidi watumishi wetu na zoezi hili litausisha watumishi waote wakiwepo Polisi lakini upande wa Majeshi (JWTZ) wao wataandaliwa utaratibu wao wakati mwingine” , amesema

Aidha Mhe Kairuki amewataka Watumishi kote nchini katika Wizara mbalimbali, Idara za serikali zinazojitegemea, Tawala za Mikoa na mamlaka za serikali za mitaa, Wakala za Serikali, Taasisi na mashirika ya Umma ambapo zoezi zitahusisha na watrumishi wa serikali kwa upende wa Zanzibar.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA Bwana Mohamed Hamisi amesema tayari wameandaa watumishi 400 kwaajili ya zoezi hilo kwa nchi nzima ambapo BVR zaidi ya 5000 zitatumika.






Kategori

Kategori