TANZANIA KINARA KWA BIASHARA HARAMU YA BINADAMU DUNIANI


Nchi ya  Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa mataifa yanayoshamiri  kwa biashara haramu ya kusafirisha binadamu kwa ajili ya utumwa wa ngono duniani.

Hayo yamelezwa leo jijini Dar es Salaam na Katibu wa Sekretarieti ya Kitaifa ya kuzuia na kupambana na biashara haramu ya bianadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Bw. Separatus Fella alipokuwa akiongea katika mkutano uliondaliwa na shirka la kimataifa la msaada wa sheria (NOLA) kwa lengo la kutoa elimu juu ya mdahara ya kusafirisha watoto.

"Tanzania ni kusudio,mkondo na chanzo cha usafirishaji wa wanawake na watoto wanaopelekwa kwenye biashara ya utumwa wa ngono katika mataifa mengine, na hii ni kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa nchini Marekani"

Bw. Fella amesema wasafirishaji binadamu wamekuwa wakitumia Tanzania kama chanzo cha kupitisha na kupata watoto wanawake wakufanya biashara hiyo na kuwa serikali itaandaa takwimu za watu walioathirika na usafirishaji huo.

WAZIRI WA ELIMU ATAKA VETA KUUNGANA NA COSTECH


WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako amesema kwa mwaka huu wa fedha, wamejipanga kuhakikisha wanafufua karakana zilizopo na kuhakikisha zinaendana na matakwa ya serikali ya Viwanda.

Akizungumza wakati alipotembelea katika banda la VETA, Ndalichako alisema pamoja na kufufua karakana zilizopo Veta pia wataongeza wigo wa kuhakikisha zinakuwa nyingi na kuboreshwa.

Alisema kazi inayofanywa na VETA ni kubwa ila tatizo lipo kwenye kujitangaza ili kuweza kuuza bidhaa zao.
"Kazi wanayofanya Veta ni kubwa, lakini changamoto ipo kwenye kujitangaza, bado hawajajitangaza katika kutoa huduma zao. Hivyo tutashirikiana na Costech ili kuendeleza VETA na kupunguza kuagiza vitu kutoka nje ya Nchi," alisema.

Ndalichako alisema tatizo linalosababisha la Veta kuwa chache ni gharama zake kwani jengo moja linagharimu bil. 9, hivyo wameshawaagiza Veta kupitia upya gharama kwa viwango tofauti tofauti ili kupata Veta nyingi.

TECHNO YAJA NA SMARTPHONE YA CAMON 9, WATEJA 100 WA MWANZO WAZIGOMBANIA

 Kampuni ya simu ya Tecno yazindua Smartphone ya Camon 9 nchini Tanzania 

• Ina kamera yenye uwezo wa mega pixel 13 

•Yaja na  ofa ya GB 10 kutoka kampuni ya simu ya Vodacom kwa muda wa mwezi moja.


Meneja wa mauzo wa TECHNO Bw Fred Kadilana akielezea ubora wa CAMON c9


Kategori

Kategori