MAUAJI YA ALBINO YAIBUKA KWA KISHINDO. DKT MENGI ATOA MILIONI 10 WAUWAJI WAKAMATWE: SERIKALI NAYO ICHUKUE HATUA KUKOMESHA MAUAJI HAYO.

MAUAJI YA ALBINO YAIBUKA KWA KISHINDO. DKT MENGI ATOA MILIONI 10 WAUWAJI WAKAMATWE: SERIKALI NAYO ICHUKUE HATUA KUKOMESHA MAUAJI HAYO.

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/7e5cebf75b882ff6cf47e51c7f3ca25d_XL.jpg 
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi amesema kuwa atashirikiana na jeshi la Polisi nchini Tanzania Kutoa zawadi ya shillingi millioni kumi kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa watu waliyomkata mkono Munghu Mugasa mwanamke mwenye ulemavu wa ngozi katika kijiji cha Buhekela Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora pamoja na kumuua mume wa mama huyo nakujeruhi watoto wao wawili.

Dkt. Mengi ameyaeleza hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akiongea na vyombo vya habari na kueleza kuwa IPP itachukua jukumu la kuwasomesha watoto wawili wa familia hiyo ambao baba yao ameuwawa na mama yao kuachwa na ulemavu huku akilitaka jeshi la Polisi nchini kuhakikisha kuwa wanawatia nguvuni wale wote waliohusika na tukio hilo. 
“Unge jiskiaje endapo aliye uwawa angekuwa ndugu yako ama aliye katwa mkono ni ndugu yako? Inasikitisha sana. Mimi sina la kufanya ila naomba sana serikali na hasa jeshi la polisi Mkoa wa Tabora kufanya msako kuwakamata waliohusika na tukio hili lakusikitisha” Amesema Dkt Mengi.

"UNYWAJI WA POMBE NA UVUTAJI WA SIGARA  KILA SIKU HULETA KISUKARI"

"UNYWAJI WA POMBE NA UVUTAJI WA SIGARA KILA SIKU HULETA KISUKARI"

http://www.prevention.com/sites/default/files/EatToBeatDiabetesGoGuide-620px.jpg
Wizara ya afya na ustawi wa jamii nchini Tanzania imebaini asilimia 13.7 ya wananchi wanadalili ya ugonjwa wa kisukari kwa Tanzania bara hali inayosababishwa na uvutaji wa sigara au tumbaku na unywa wa pombe kupita kiasi pamoja na kutokufanya mazoezi na lishe duni.

Utafiti huo pia umeonyesha kuwa asilimia 14.5 wanakunywa pombe kila sikuhuku asilimia 36 wanavuta sigara. Kuhusu masuala ya uzito kupita kiasi ni asilimia 24 wanauzito usio hitajika huku asilimia 30 wameonekana kuwa na ongezeko la msukumo wa damu.

Akizungumza wakati akizindua utoaji wa huduma za bure zinazotolewa na Jeshi la wananchi wa Tanzania(JWTZ) kuelekea kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya jeshi hilo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam kwa muda wa siku 3, Kaimu mkurugenzi wa tiba wa wizara hiyo Dr.Ayoub Magimbu amewataka wananchi kuipunguza matumizi ya vitu ambavyo vitahatarisha maisha yao.

Kategori

Kategori