MWANAJESHI WA JWTZ ALIYE UWAWA DRC AZIKWA LEO MAKABURI YA KISUTU

MWANAJESHI WA JWTZ ALIYE UWAWA DRC AZIKWA LEO MAKABURI YA KISUTU



Mwili wa askari aliyeuawa kwa kupigwa risasi Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC Afisa Luteni Ahmad Rajab Mlima umeagwa na kuzikwa leo katika makaburi ya kisutu jijini Dar Es Salaam.

Mwili huo uliagwa katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Lugalo ambapo heshma za kijeshi zilitolewa kisha mwili huo kupelekwa nyumbani kwao Mbezi Beach kwaajili ya kuagwa na familia kisha kupelekwa katika makaburi ya Kisutu kwa maziko.

CHUO CHA HESABU KUANZISHWA HAPA NCHINI


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa hapo jana amekutana na kufanya 
mazungumzo na Wajumbe wa African Institute for Mathematical Sciences – Next Einstein Initiative kuhusu kuanzishwa kwa Chuo cha AIMS - NEI hapa Tanzania.

Wajumbe hao walimtembelea Waziri Kawambwa ofisini kwake  kufuatilia kunzishwa kwa  chuo hicho hapa nchini.  Waziri Kawambwa ameuhakikishia ujumbe huo kuwa Serikali ya Tanzania itatekeleza kikamilifu  wajibu wake katika mchakato wa  kuanzisha chuo hicho.

KAMATI YA UCHAGUZI YATANGAZA WAGOMBEA TFF

KAMATI YA UCHAGUZI YATANGAZA WAGOMBEA TFF



Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza orodha ya mwisho ya wagombea wa uchaguzi wa TFF na wa Bodi ya Ligi (TPL Board) utakaofanyika baadaye mwezi huu.

Uchaguzi wa Bodi ya TPL utafanyika Oktoba 25 mwaka huu wakati ule wa TFF utafanyika Oktoba 27 mwaka huu. 

Kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa TPL Board na ule wa TFF zimeanza leo (Oktoba 18 mwaka huu) zitamalizika siku moja kabla ya uchaguzi saa 10 kamili alasiri.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Hamidu Mbwezeleni amewataja wagombea kwa upande wa TPL Board kugombea uenyekiti ni Hamad Yahya Juma (Mtibwa Sugar), Makamu Mwenyekiti ni Said Muhammad Said Abeid (Azam). Wanaowania ujumbe wa Bodi ya Uendeshaji ni Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui).

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA KODI KWA BIDHAA ZA SAMANI ZINAZO AGIZWA NJE

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA KODI KWA BIDHAA ZA SAMANI ZINAZO AGIZWA NJE

Serikali imeshauriwa kuongeza kodi katika bidhaa za samani zinazoingizwa hapa nchini ili kuweza kuongeza dhamani ya soko la samani zinazo tengenezwa hapa nchini na kuwawezesha wabunifu wa ndani kujiongezea kipato.

Akiongea katika mahafali ya kuhitimu kwa wanafunzi wa chuo cha ufundi cha Mtakatifu Gasper pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne katika shule hiy Mkuu wa chuo hicho Padri Achileus Mutalemwa amesema kuwa ni vyema serikali ikatambua kuwa samani kutoka nje ni chanaga moto kubwa kwa watanzania wao jishugulisha na fani hiyo.

SHIRIKISHO LA KISIASA LA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI, TANZANIA YATAKA WANANCHI KUKUBALI

SHIRIKISHO LA KISIASA LA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI, TANZANIA YATAKA WANANCHI KUKUBALI


Serikali ya Tanzania imesisitiza kuwa haitokubali kushiriki mpango wowote wa kuharakisha uundwaji wa shirikisho la kisiasa la nchi za Afrika Mashariki pasipo ridhaa ya wananchi wake.

Taarifa kutoka ndani ya wizara ya Afrika Mashariki zimesema,


Hatua hiyo ya Tanzania inatokana na mpango unaoendeshwa hivi sasa na nchi za Rwanda, Kenya na Uganda wa kutaka kuundwa kwa shirikisho hilo ifikapo mwaka 2015.

Taarifa ya waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki nchini Tanzania mhe. Samuel Sitta inayosema kuwa itashangaza sana iwapo shirikisho litakaloundwa pasipo ridhaa ya wananchi na kuwa itakuwa ngumu kwa shirikisho hilo kudumu, kutokana na mifano mingi kama nchi za Misri, Syria na Libya kushindwa kuunda shirikisho hilo.

WANANCHI 40,000 WALIA NA TATIZO LA MAJI HUKO ARUMERU

WANANCHI 40,000 WALIA NA TATIZO LA MAJI HUKO ARUMERU



Wananchi zaidi ya 40,000 wa vijiji 30 katika wilaya za Arumeru na Longido mkoani Arusha wanakabiliwa na tatizo kubwa la kukosekana kwa maji katika maeneo yao kutokana na uharibifu mkubwa wa vyanzo vya maji unaoendelea katika maeneo yao

Vyavyo vya maji vilivyo adhirika katika chemchem zinazotoka katika msitu wa mlima Meru huku serikali ikiombwa kuchukua hatua za haraka kukabiliana na tatizo hilo.

Uharibifu huo umefanyika katika kata ya ngarananyiki ambapo wananchi na viongozi wa kata hiyo wamesema pamoja na kufanya jitihada za kudhibiti tatizo hilo bado linaendelea nakuomba serikali katika ngazi za juu kuliangalia suala hilo kabla madhara hayajawa makubwa

Wananchi waliotoa ombi hilo ni pamoja na Julius Ayo, Furaha Mungure na Barnaba Simon, ambapo wamesisitiza kuwa kuharibiwa kwa vyanzo hivyo ndio chanzo cha hatari ya kukosekana kwa maji safi na salama katika maeneo yao

WALIOKOPESHWA NYUMBA ZA SERIKALI WAPEWA MWEZI MMOJA, UJENZI WA ZINGINE 851 NAO UMEANZA


Waziri wa ujenzi nchini Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa kipindi cha mwezi mmoja kwa watumishi wa umma waliokopeshwa nyumba za serikali, kulipa madeni yao vinginevyo watanyang'anywa nyumba hizo na kupewa watumishi wengine.


Waziri Magufuli ametoa agizo hilo leo muda mfupi baada ya kuzindua ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa eneo la Mabwepande nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, nyumba zitakazopokeshwa kwa watumishi wa umma.

Katika maelezo yake, waziri Magufuli amesema takribani wafanyakazi 2500 bado hawajalipa madeni wanayodaiwa, ambapo amemuomba makamu wa rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal kuunga mkono hatua hiyo ya kutoa mwezi mmoja au kuwanyang'anya nyumba wadaiwa hao.

Wakati huohuo, makamu wa rais Dkt Mohammed Gharib Bilal, amesema muungano wa Tanganyika na Zanzibar utaendelea kudumu licha ya njama za watu wachache wanaotaka muungano huo uvunjike.
  MCHAKATO WA KATIBA MPYA: JK,LIPUMBA,MBATIA NA MBOWE WAJADILI IKULU

MCHAKATO WA KATIBA MPYA: JK,LIPUMBA,MBATIA NA MBOWE WAJADILI IKULU


 
KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete mchana wa leo, Jumanne, Oktoba 15, 2013 ameanza kukutana na viongozi wa siasa vyenye Uwakilishi Bungeni kujadili maendeleo ya mchakato wa Katiba Mpya nchini.

Viongozi wanaoendelea kukutana na Mheshimiwa Rais Kikwete, Ikulu, Dar es Salaam sasa katika mazingira maelewano na mwafaka, ni Mwenyekiti wa Chama cha CUF Mheshimiwa Ibrahim Lipumba ambaye ndiye msemaji wa viongozi hao, Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mheshimiwa James Mbatia.

Wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Mheshimiwa Philip Mangula, Mheshimiwa Isaack Cheyo ambaye anamwakilisha Mwenyekiti wa Chama cha UDP Mheshimiwa John Cheyo na Mheshimiwa Mrindoko ambaye anamwakilisha Mwenyekiti wa TLP Mheshimiwa Augustine Mrema. Waheshimiwa John Cheyo na Mrema wako nje ya nchi.

Pamoja na viongozi hao pia yuko Mheshimiwa H. Mnyaana Bwana Julius Mtatiro wa Chama cha CUF, Waheshimiwa Tundu Lissu na John Mnyika wa CHADEMA na Bwana Martin Mng’ongowa NCCR - Mageuzi.

Kategori

Kategori