OBAMA KUPEWA TUZO NA CHUO KIKUU HURIA, SHAHADA YA UCHUMI NAYO YAANZISHWA

OBAMA KUPEWA TUZO NA CHUO KIKUU HURIA, SHAHADA YA UCHUMI NAYO YAANZISHWA


Chuo kikuu Huria cha Tanzania (CKHT) Kitamtunuku Rais Barack Obama shahada ya heshima au uzamivu iitwayo Doctor of Lettres (D.Litt) Henoris kwa mheshimiwa Raisi wa Marekani Barack Obama kwa kutambua mchango wake mkubwa katika maisha ya binadamu.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Tolly Mbwete amesema shahada hiyo ya Obama imetokana na kutambua mchango wake katika fani ya maendeleo ya kiuchumi ya jamii ( Community Economic Development).

"Shahada hii sio ya kwanza kuitoa, na hii itakuwa ya 7 kutoa hapo hawali tuliwahi kupata msaada kutoka katika serikali yake ilikuweza kuanzisha shahada hii hapa nchini hivyo itakuwa vyema kama akifahamu maendeleo ya chuo hicho" Alisema 

Akitaja waliowahi kupewa tuzo na Chuo hicho kuwa ni Rais mstaafu wa Afrika Kusini Bwana Nelson Mandela, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Benjamini Mkapa, Alli Hassan Mwinyi 

Wengine ni Dr. Jane Goodall ambaye ni mtafiti wa mambo ya Sokwe mtu huko Afrika Mashariki na Profesa wa mawasiliano wa Uingereza Bwana David Mellor, chuo hicho kikiwa cha kwanza kufundisha masomo ya uzamili ya maendeleo ya kiuchumi ya jamii huku kikidahili wanafunzi wa shahada ya uzamili ya sayansi ya maendeleo ya kiuchumi ya jamii

Prof. Mbwete amesema kwa mwaka ujao wa masomo yaani 2013/2014 chuo hicho kitaanza kutoa Vyeti, Shahada ya kwanza na Stashahada ya uzamili ya maendeleo ya kiuchumi ya jamii kutokana na umaarufu wa mafunzo hayo. Alisema 

"Kuanzisha shahada hii itawezesha wananchi kujua elimu ya kutafuta fursa za kiuchumi na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja katika jamii yetu"Alisema Prof. Mbwete

FURSA ZA AJIRA ZATAJWA NA MTANDAO UNAO TOA AJIRA FEKI NAO WAPONDWA

FURSA ZA AJIRA ZATAJWA NA MTANDAO UNAO TOA AJIRA FEKI NAO WAPONDWA

Sekretariet ya Ajira nchini imeainisha fursa za ajira zilizopo serikali na kuwataka wahitimu au wanafunzi wanaopata fursa ya kujiunga na elimu ya juu kukimbilia fursa hiyo ilikutatua tatizo la ukosefu wa ajira baada ya kuhitimu

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam, Katibu Sekretariet ya Ajira bwana Xvavier David amesema fursa hizo zipo kwa wingi lakini wanafunzi wengi hupuuzia swala hilo nakujikuta katika ukosefu wa ajira

“Kuna nafasi za ajira kwenye Ualimu, Utabibu, Afisa utendaji, Kilimo ambazo wahitimu wake sio wengi na nafasi za Ajira zipo nyingi hivyo niwatake wahitimu kukimbilia huko nasiokuwa wote tutakumbilia taaluma zilezile baadae ajira zina kosekana”Alisemai ikiwemo mitandao ya kijamii

Aidha, Xvavier David amekanusha vikali taarifa zinazotolewa na mtandao wa www.eastafricajobscareer.com lenya tangazo zinalosema KAZI UTUMISHI JULAI 2013, pamoja na KAZI UTUMISHI AUGUST 2031 JOB IN TANZANIA" kuwa sio ya kweli na kwamba huo ni upotoshaji

"Huu ni upotoshaji mkubwa kwa kuwa matangazo hayo yanasababisha usumbufu mkubwa kwa umma, na tumekuwa tukisumbuliwa mara kwa mara wakati sekretariet  ya Ajira haijatoa matangazo haya na tovuti hiyo inafanya hivyo kwaajili ya kujipatia fedha hivyo wajihadhari na matapeli hao" alisema Xvavier

Tungeomba watembelee tovuti yetu ya www.ajira.go.tz ambayo inamatangazo yetu au wapige simu no. 255 - 687624975 ili kupata habari na taarifa sahihi za ajira hapa nchini, na kuwa wanafanya mchakato wa kuwatambua wamiliki wa tovuti hiyo ili waweze kuongea nao juu ya swala hilo. Alisema Xvavier

Naomba kufahamisha umma kuwa sekretariet ya Ajira aiwajibiki nawala haitawajibika kwa taarifa ama matangazo yanayohusu Ajira Serikalini katika vyombo mbalimbali vya habari, hivyo nawataka wote wanaoendelea kutoa matangazo hayo ua uongo/kughushi yenye lengo la kupotosha umma kuacha maramoja. Alisema Xvavier

Hatahivyo, Xvavier amewaomba wale wote walioomba ajira katika usaili wa tangazo la kazi lililotolewa tarehe 26 Machi, 2013 kuwa wale wote ambao wamekidhi zigezo vya Ajira yatatolewa katika mtandao wa sekretariet ya Ajira wiki ya kwanza ya mwezi Julai 2013 hivyo kuwataka kutembelea mtandao wa ajira kupata tarifa zaidi

Xvavier amesema kuwa wanaoomba kazi serikalini watambue kuwa fursa za Ajira ni za ushindani nakuwa sasa hivi watu niwengi na serikali inahitaji watumishi wenye uwezo wa kitaaluma na kiutendaji ili kuweza kuwahudumia watanzania. 

SABASABA KWA PAMBA MOTO, NCHI 32 ZITASHIRIKI HUKU MAKAMPUNI 1620 YA NDANI NAYO YATAKUWEPO


NCHI 32 pamoja na makampuni ya ndani 1620 yatashiriki katika maonyesho ya 37 ya biashara ya kimataifa yajulikanayo kama sabasaba yanayofanyika kila mwaka jijini Dar es salaam, katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuanzia tarehe 28 june mpaka tarehe 8 julai mwaka huu.


Akiongea na wanahabari katika viwanja hivyo, Kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania (TANTRADE) Bi. Jackline Malekwe amesema maonyesho ya mwaka huu yana mabadiliko mengi tofauti na miaka iliyopita.



Katika mwaka huu kutakuwa na mabanda ya Nchi na bidhaa zake huku Tanzania ikiwa na Bandalake ambalo litakuwa na bidhaa za Tanzania (Made in Tanzania) kwa lengo la kuinua biashara ya vitu vinavyo zalishwa hapa nchini. Alisema Bi Jackline

Aidha Bi Jackline amesema mamlaka ya maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imepewa wajibu wa kuhakikisha wanakuza wajasiriamali wote nchini na kutoa fursa za biadhaa zao ili kukuza uchumi, na kwamba fursa ya Sabasaba kwa wajasiriamali nikujifunza na kuiga yale watakayo ona wengine wanafanya ilikukuza ufanisi wao


Tayari Maandalizi yame kamilika kwa baadhi ya Mabanda katika viwanja hivyo, ambapo kibanda cha HOME SHOPPING CENTER tayari kilisha pendeza sana na maandalizi yamekamilika


Wakati huo huo Watanzania wametakiwa kuhudhuria maonyesho hayo kwa nia ya kujifunza mambo mbalimbali na siyo kutembea bila ya kujifunza chochote, amesema Bi. Fatma Washoto ambaye ni Meneja masoko wa Home Shopping Centre.


Katika maonyesho haya kutakuwa na utaratibu mpya wa kukata tiketi kutumia mashine, hivyo mtu anaweza kwenda katika maeneo kama Steers - Mkabala na Makumbusho, Mlimani City na katika viwanja hivyo, hii nikutokana na kuondoa usumbufu Getini . 

Bi. Jackline alisema kuwa tayari Tiketi za kujiunga na maonyesho ya mwaka ujao 2014 zinatolewa na mamlaka hiyo.
DAWA ZA KULEVYA NI JANGA LA TAIFA, YADAIWA KUWAHUSISHA MATAJIRI NA VIGOGO

DAWA ZA KULEVYA NI JANGA LA TAIFA, YADAIWA KUWAHUSISHA MATAJIRI NA VIGOGO

Wakati Tanzania ikiungana na nchi zote duniani katika maadhimisho ya kupiga vita Dawa za kulevya. kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika mkoani Dodoma

Taifa bado lina kabiliwa na changamoto kubwa ya kudhibiti matumizi ya dawa hizo kutokana na wimbi kubwa la vijana kuendelea kujiingiza katika matumizi ya madawa hayo, hali ambayo inatikisa mustakabali wa mendeleo ya taifa 

Matumizi ya madawa haya yana ambatana na matukio ya uhalifu, uzururzji na maambukizi ya virusi vya ukimwi ambavyo vinaongezeka siku hadi siku

Akiongea katika maadhimisho hayo, Waziri wa nchi ofisi waziri mkuu sera na uratibu wa Bunge Mhe. Wilium Lukuvi kwa niaba ya Waziri mkuu Mhe. Mizengo Pinda amesema matumizi ya dawa za kulevya ni janga kwa taifa kutokana na vijana wengi hasa walioko shuleni

"Hali hii inatishia mustakabali wa taifa, vijana wengi walioko mashuleni wanazidi kujiingiza kwenye matumizi ya dawa hizo" Alisema Lukuvi

Aidha Mhe. Lukuzi amesema Vita didhi ya matumizi na biashara haramu ya madawa ya kulevya inahitaji ushirikiano wa hali ya juu kwa Watanzania wote kwani Tayari imeshaanza kulichafua jina la Tanzania katika nchi mbalimbali Duniani

Hatahivyo Tume ya Kuratibu udhibiti wa dawa za kulevya kupitia Kamishna wake Bwana Christopher Sekiondo amesema, tume hiyo inakabiliwa na chanagamoto kubwa katika kutekeleza majukumu yake kutokana na biashara ya dawa za kulevya kuhusisha watu wengi wakiwemo wenye nyadhifa za juu na matajiri

" Biashara ya madawa ya kulevya ningumu kutokana na kuwahusisha watu wengi wakiwemo wenye nyadhifa za juu na matajiri" Alisema Bwana Sekiondo

Siku ya kupinga vita ya dawa za kulevya Duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 26 mwezi juni ambapo Tanzania iliungana na mataifa mengine katika kukemea Madawa hayo

Tangu mwaka 1999 maadhimisho hayo hufanyika Duniani, huku kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa ni FURAHIA AFYA YAKO NA SIYO MADAWA YA KULEVYA


WANANCHI WA AFRIKA KUSINI WAENDELEA KUMWOMBEA MANDELA

WANANCHI WA AFRIKA KUSINI WAENDELEA KUMWOMBEA MANDELA

    

Hali ya Raisi wa kwanza mweusi nchini Afrika kusini Nelson Madiba Mandela mwenye umri wa miaka 94, imeelezwa kuwa ni mbaya na amekata kauli huku wananchi wan chi hiyo wakiendelea kumwombea

Hapo jana Ikulu ya Afrika Kusini kupitia Rais wake bwana Jackob Zuma ili tangaza kuwa hali ya Raisi huyo mstaafu kuwa ni mbaya,  ikiwa ni mara ya kwanza kwa Raisi huyo kujitokeza hadharani nakukiri kwamba hali ya Mandela sio nzuri

Rais Jackob Zuma aliwatangazia wananchi wake kujiandaa kusherehekea sherehe ya Raisi Mandela ambayo ni mahususi kama kumuenzi ifikapo Julai 18 ambayo ni tarehe ya kuzaliwa kwa muasisi huyo.

“We must all be planning what to do next month in marking our 67 minutes of doing good for humanity as called upon by Madiba to do so, when he lauched the International Mandela Day Campaing”Zuma said Let us make it the biggest Mandela Day ever on the 18 of July on doing good all over the country


Habari zilizo chapishwa na vyombo vya habari mbalimbali  nchini humo zinasema kuwa ndugu walionekana wakiiingia Hosptalini  humo lakini bila kusema chochote, na zaidi ni kuwa Familia ya Mandela ili kaa kikao hapo jana huko Qunu eneo ambalo aliko kulia Raisi huyo lakini yaliyo zungumzwa bado ni siri ya familia yake.

Katika sherehe iliyoandaliwa na nchi hiyo ambayo itafanyika tarehe 18 Jully ambayo itakuwa mahususi kwaajili ya matendo mema kwa jamii ndani ya nchi hiyo ndio tarehe ya kuzaliwa kwa Mandela ambapo atatimiza miaka 95. 

UJENZI WA BARABARA WA WAONDOA MACHINGA ENEO LA MANZESE

Wafanya biashara wadogo kandokando ya barabara ya Morogoro eneo la Manzese jijini Dar es salaam wameendelea kutolewa kwa nguvu chini ya ulinzi mkali wa Polisi na wanamgambo ilikupisha ujenzi wa barabara hiyo


Blog hii ili mtafuta mkuu wa Wilaya wa Kinondoni bwaba Jordan Rwegimbana nakueleza kuwa, wafanyabiashara hao wanaondolewa kupisha ujenzi wa barabara hiyo kwani mkandarasi anaye jenga barabara hiyo alilalamikia kuwepo kwao katika eneo hilo kuwa unakwamisha ujenzi wa barabara hiyo

 "Wilaya ya Kinondoni inamasoko 30, hivyo wafanyabiashara wangeenda huko kufanya biashara mahali ambapo pako sahihi kisheria"Alisema Rwegimbana



Swala la kuwepo uvumi kuwa zoezi la kuwaondoa wafanya biashara hao kunatokana na ujio wa Rais Barack Obama wa marekani, bwana Rwegimbana alikanusha kuwa jambo hilo haliwezekani kwani nimuda sasa wamekuwa wakishugulikia swala la kuwaondoa wafanyabiashara hao katika eneo hilo

 

Kutokana na madai ya wafanyabiashara kulaumu kupotelewa mali zao Bwana Rwegimbana amewataka wafanyabiashara hao kuripoti kwake mara moja ilihatua ziweze kuchukuliwa


Barabara hiyo inajengwa tokea Ubungo mpaka Posta, ikiwani ya ujenzi wa magari ya endayo kasi nchini

MAIZE DESEASE WORRIES FARMERS IN TANZANIA

When the Government plan to give a statement this week on the magnitude of the "Maize Lethal Necrosis- (MLN)" this week Thecampasvision Blog Bring you the Brief about the causes of the Disease as written by The International Institute of Tropical Agriculture (IITA) in Dar es salaam.

The disease has already affected Manyara, Mara, Kagera and Arusha Regions in Tanzania. The Minister for Agriculture,Foood security and Cooperatives Eng. Christopher Chiza will give out effects of the Disease in country.





DANCE 100% YA ANZA KWA KISHINDO VIWANJA VYA TCC CHANG'OMBE,

Mashindano ya Dance yanayo fanywa na kituo cha utangazaji cha EATV yanayo kwenda kwa jina la DANCE 100% yameanza tena kwa kishindo huku makundi kibao yakijitokeza kuwania nafasi ya kushiriki mashindano hayo ambapo mshindi atajinyakulia pesa taslimu Millioni 5.


Katika kujiandikisha kwa awamu ya kwanza uliofanyika katika viwanja vya TCC Chang'ombe, jumla ya makundi 15 yalijitokeza siku hiyo ambapo makundi 5 tu ndio yalishinda kuingia katika mashindano hayo, Kumbuka mashindano haya yatarushwa hewani na kituo hicho kuanzia saa 1 jioni siku ya jumatano.



Makundi yaliyoshinda ni Ikulu Vegas, Ganzi More Fire, The Chocolate, D.D.I Crew na The W.T kati ya makundi 15 yaliyojitokeza uwanjani hapo


Makundi mengine yaliyoshiriki lakini hayakuibuka kidedea ni Mtwara Dancers, SMB, Black Winners, Moa Dancers, Wakali Popote, Waku shine, Black Texas, The new black, NB Ndala na Leo Tena,

Katika hamu hii Dance 100% haitachukua wakali wa Wilaya ilikuweza kuwapa nafasi kila kundi litakalo penda kushindana. Awamu ya pili itafanyika viwanja vya Don Bosco Oyster bay siku ya tarehe 30. 6. 2013 kuanzia hasubuhi.


Shindano hili linasimamiwa na majaji watatu ambao nao ni wataalamu wa ku Dance wakiongozwa na Lotus Kyamba, Supa Nyamwela na Adam Juma, huku ikisindikizwa na watangazai bora kabisaaa Saigon na Babs.


Dance 100% ya mwaka 2012 kundi la T Africa liliibuka kidedea na kujinyakulia kitita cha Millioni 5 kutoka EATV ambapo awamu hii mshindi atajinyakulia kiasi hichohicho cha Millioni 5. mashindano haya yanafanywa na kituo cha utangazaji cha EATV.

JOTO HASIRA ITAISHALINI- FOLENI NJIA NZIMA

Watumiaji wa barabara ya New Bagamoyo Road hatuna nafuu hata kidogo licha ya barabara hiyo kufunguliwa na kuruhusu njia mbili kutumika baadhi ya maeneo

Poleni kuanzia Makongo - Mwenge, new bagamoyo roada

Kwa muda wa wiki mbili sasa tunalala na usingizi kabisa pindi tunapofika Maeneo ya Makongo mpaka kuishika Mwenge, unatumia zaidi ya dakika 45 eneo mojatu. Kama daraja la kwanza eneo hilo limekamilika basi lifunguliwe kama ilivyo maeneo mengine ilituweze kuwahi makazini.

New Bagamoyo Road asubuhi hii- picha na Campasvision

New bagamoyo Road inatarajiwa kukabidhiwa kwa serikali ifikapo mwezi wa nane licha yakuwepo kwa  maeneo mengi ambayo hayajakamilika hadi hivi sasa hasa madaraja ya upande mmoja wa barabara hiyo


Barabara hii haina aina matuta mwanzo mwisho, hala za barabarani baadhi ya maeneo tu, vituo havieleweki nikama vimewekewa Bajaji lakini chakushangaza hadi kilimani kuna kituo cha daladala mwanzo wa mteremko kituo. mkandarasi wa hii barabara amefanya vyema kwa upande wake

WAZIRI MKUU WA TANZANIA ARUHUSU POLISI KUPIGA RAIA

WAZIRI MKUU WA TANZANIA ARUHUSU POLISI KUPIGA RAIA

Photo: HOTMIX (11:00 Jioni) Polisi wakabidhiwa rungu, watakiwa kushusha kichapo kwa kila mtu atakaye waletea ubishi... Hiyo ni kauli kutoka kwa Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda leo Bungeni, Una maoni gani kuhusu hilo?

Pia, tuko na mkemia mkuu wa serikali, Je, unajua ni perfume na deodorant za aina gani zinazoweza kukusababishia kansa? Uliza maswali yote yanayohusu vipodozi, perfume, DNA na dawa mbalimbali utapata majibu HAPA!

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda amewakabidhi rungu Jeshi la Polisi ilikupiga raia ambao watajikusanya au kuandamana bila kibali cha Jeshi hilo

Akijibu maswali ya papo ka hapoambayo huyajibu kila Alhamisi Bungeni, Waziri mkuu huyo amesema Polisi wapige tu raia wakati akijibu swali lililo ulizwa na Mbunge wa Kilwa Mhe. Murtaza Mangungu aliye taka kujua serikali inachukua hatua gani kwa Polisi wanao piga raia

Mhe. Pinda alijibu kuwa,
“Ukifanya fujo na umeambiwa usifanye hiki na ukafanya fujo na ukakaidi ukafanya fujo  utapigwa tuu, hakuna maana nyingine, nilazima tukubaliane kuwa nchi hii ina endeshwa na misingi ya kisheria  sasa kama wewe umekaidi hutaki unaona kama nijeuri na zaidi wewe ndio jeuri zaidi utapigwa tuu na mimi nasema wapigeni tuu maana hatuna namna nyingie” alisema kwa msisitizo waziri huyo

Waziri mkuu aliongeza kuwa, Mara ya mwisho hapa Bungeni nilisema nataka kurudisha hali ya amani na nilisema nilazima turudishe amani sasa tuache tusiwakamate wakati wanavunja amanani, nyiye wenyewe mtasema tunawaachai” Alisema

Aidha Kauli hiyo ya Waziri iliyosindikizwa na makofi ya Wabunge… ilikuwa tofauti kwa Mbunge wa Konde Mhe. Khatibu Saidi Hadji aliyetaka Waziri huyo kujibu ni kwanini amevunja katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 13 kifungu cha 6-B na 6-E

Kifungo hichi kinasema kuwa, NIMARUFUKU KWA MTU YEYOTE ALIYESHATAKIWA KWA KOSA LA JINAI KUTENDEWA KAMA MTU MWENYE KOSA HILO, NI MARUFUKU KWA MTU YEYOTE KUTESWA, KUADHIBIWA KINYAMA AU KUPEWA ADHABU ZINAZOTWEZA UTU NA KUMDHALILISHA jambo ambalo Waziri alijibu kama ifuatavyo

Waziri mkuu alijibu kuwa, Lazima uweke tofauti kwa mtu aliye kamatwa na mtu ambaye anavunja sheria, kama wewe umeambiwa usiende kufanya maandamano ukaenda nilazima tufanye hivyo, na nilazima utii sheria bila shuruti. Alisema Mhe Pinda

Kwa muda sasa kumekuwa na taarifa hasa maeneo kunakotokea maandamano na vurugu, Raia kulalamikia polisi kuwa piga hata kuwa teas… ambapo Waziri mkuu kawakabidhi rungu kuwapiga raia

 Naogopa jamani nahisi kama bado kidogo hakuta kucha TZ


MAMLAKA YA ELIMU YAGAWA MADAWATI 420 KWA WILAYA YA MASASI - MTWARA

MAMLAKA YA ELIMU YAGAWA MADAWATI 420 KWA WILAYA YA MASASI - MTWARA




Mamlaka ya Elimu nchini imetoa jumla ya madawati 420 kwa shule za msingi 12 katika wilaya ya masasi mkoani Mtwara yenye jumla ya shilingi Millioni 79 nakuweza kupunguza upungufu wa madawati katika wilaya hiyo

Akiongea na Blog hii katika ofisi za mamlaka hiyo hii leo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkurugenzi wa TEA bi. Sylvia Lupembe amesema madawati hayo yamepunguza upungufu kutoka asilimia 22 hapo awali mpaka kufikia asilimia 17 hivi sasa

“Wilaya yote ya Masasi ilikuwa na upungufu mkubwa wa madawati lakini kwakuanzia tumeanza na idadi ya madawati 420, na hii ni awamu ya kwanza tunategemea kupeleka awamu ya pili hukohuko Masasi” alisema Lepembe

Aidha bi Sylvia Lupembe amewaomba wafadhili mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kusaidia mamlaka hiyo katika mambo mbalimbali kama ujenzi wa Madarasa, vitabu pamoja na madawati ili kuweza kuinua sekta ya Elimu nchini

“Tuchangie elimu yetu kupitia mfuko wa Elimu ili kuweza kuboresha miradi ya elimu hapa nchini, na tunapokea hata kwa wafadhili wa nje pia wandani na kushirikiana nao vyema,”Alisema Lupembe

Mkoa wa mtwara ambako wilaya ya masasi unapatikana ni miongoni mwa mikoa inayofanya vibaya katika matokea ya kidato cha nne na shule za msingi kutokana na ukosefu wa vitendea kazi kwa walimu, madarasa vitabu hata madawati.

OFISI YA SERIKALI YA MTAA MZIZIMA INAHITAJI MAREKEBISHO



Hii ndio ofisi ya mwenyekiti serikali ya mtaa makumbusho - Mzizima kiukweli inahitaji marekebisho ili kuweza kuendesha shuguli za kijamii ipasavyo nakatika eneo linalo eleweka hata kwa mgeni anayeenda katika eneo hilo kuitaji msaada wa kiserikali

Tuamke natujali vitu vyetu kuanzia chini sio tuu Wizara au Makampuni ya serikali tu hata huku kuna watanzania. Ofisi hii irekebishwe.... Diwani na Mbunge wa eneo hili kumbukeni hapa ndio mlifanya vikao vyenu na wananchi kuomba kura hasa wale makada wenu

WABUNGE 4 WA CHADEMA NA WANANCHI 60 NA MIKONONI MWA POLISI, MHE MBOWE, TUNDU LISU HAWAJULIKANI WALIPO




Jeshi la polisi  mkoani Arusha limewakamata wabunge 4 wa chadema ambao majina yao hayajajulikana mara moja, pamoja na wananchi wengine wapatao 60 huku msemaji wa kambi rasmi ya upinzani Mhe. Freeman Mbow pamoja na Mbunge wa Singida mjini Mhe. Tundu Lisu wakiwa hawajulikani walipo baada ya polisi kutawanya wafuasi wa chama hicho

Wanachama hao walijikusanya katika uwanja wa Soweto mkoani humo wakiwaaga wale waliouwawa na Bomu hapo Juzi ambapo Polisi ilidai kuwa ni kukusanyika eneo la soweto bila kibali cha sertikali

Kwa habari ambayo Blog hii imeipata kutoka kwa shuhuda huko Arusha nikuwa hali bado ni tete na kuwa kuna majeruhi kadhaa wamekimbizwa katika Hospitali ya mount Meru kwa matibabu zaidi juu ya tukio hilo

Utapata Updates kadri tutakavyokuwa tunazipata 





Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimeichukuliwa hatua ya serikali ya kutangaza dau la shilingi Mil. 100 kwa yeyote atakaye fichua taarifa za kumtia hatia aliye husika na tukio la kurusha bomu lililo sababisha vifo vya watu 4 nakuacha wengine 50 wakiwa wamejeruhiwa vibaya

Hatua hiyo iliyopingwa na Chadema ilitangaza jana Bungeni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge Mh. Willium Lukuvi ambapo Mkurugenzi wa habari na mawasiliano Mhe. John Mnyika amesema kitendo hicho nikutumia vibaya fedha na rasilimali za serikali

Akiongea hii leo jijini Dar es salaam katika makao makuu ya chama hicho, Mhe. Mnyika amesema fedha hizo ambazo serikali imezitangaza Ingekuwa bora kama wangezitumia kuwa fariji majeruhi na waliopoteza ndugu zao katika tukio hillo, amesema Mnyika

Mnyika amesema, chama hicho kimetoa Baraka zote kwa wabunge wake kutohudhuria Bungeni mpaka pale maombolezo yatakapo malizika huko Arusha na kwamba Mbunge yeyote wachama hicho hataruhusiwa kuhudhuria Bungeni

Aidha Mhe. Mnyika ameongeza kuwa chama hicho kimesikitishwa na kitendo cha Bunge kutositisha shuguli zake kutokana na tatizo la Arusha wakati majanga kama haya yanapotokea kwani kwa mujibu wa kanuni za Bunge inaruhusiwa kusimamisha shuguli zote mpaka hali ikae sawa.

“Bunge linatumiwa na serikali kuchamazisha haki, Polisi nao wanatumika na Serikali lakini ukweli ni kwamba bado tuna muhimili wa mahakama ambayo naamini yenyewe itasimamia haki daima”alisema Mnyika.

Kuusiana na mkanda wa video ambao chama hicho inadai inamuonyesha Polisi wa kikosi cha FFU akilipua bomu hilo, Mnyika amesema watasubiri mkanda huo kupitiwa na mwanasheria kwanza na viongozi wengine wajuu wa chama hicho iliwaweze kuitoa kwa wananchi wote kuiona

“Mkanda tunao na ushahidi hupo, tusubiri taratibu za kuupitia ilituweze kuangalia hasara na faida za kuutoa kama tutaona inafaa ama laa kila mtu hatauona mkanda huo”Alisema

Chama cha CCM na CHADEMA vimekuwa vikitupiana lawama kutokana na vifo vya watu 4 vilivyo sababishwa na kulipuka kwa bomu huko eneo la Soweto, jeshi la polisi likiwa kiwa limeunda kamati kuchunguza tukio hilo

WATOTO WAOMBA SIKU YAO KUJADILI RASIMU, LHRC NAO WAZIDI KUJITOSA KUTETEA HAKI ZAO



Kituo cha sheria na haki za binadamu, hii leo kimefanya maadhimisho yake ya siku ya mtoto wa Afrika katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam wakiwa na kaulimbiu isemayo Kupinga tamaduni na mienendo hasi dhidi ya watoto ni wajibu wa jamii nzima

Akionge na waandishi wa habari katika maadhimisho hayo, Mkurugenzi mkuu wa kituo hicho Bi Helen Kijo Bisimba amesema kuwa, pamoja na kuwa wameshiriki katika mchakato wa kuhimiza haki za watoto katika katiba mpya lakini wamefurahi kuwa watoto wengi sasa wanauelewa juu ya siku hiyo pamoja na haki zao.

“ Watoto wengi sasa wanaelewa umuhimu wa siku hii, pamoja na jitihada zetu tunaamini kunamafanikio yatafikiwa, kuanzia ndani ya Rasimu na katiba yenyewe” alisema Hellen


Aidha Kamishna msaidizi wa wizara ya Afya na ustawi wa jamii bwana Rabikira Mushi amesema, ni wakati sasa kwa jamii nzima kutambua suala la kulinda haki za watoto ni la jamii nzima na kwamba kila halmashauri ina wajibu wa kulinda haki za watoto katika maeneo yao.

“Halmashauri zote zinatakiwa kujali watoto kwenye maeneo yao bila kujali huyu ni mzaliwa wa hapo au nimgeni kwani jukumu la watoto nilakwao kisheria na sio ombi, pamoja na jamii nayo itambue hilo sio kuwaachia serikali tu nilazima kila mtu ajiwajibishe juu ya kulinda haki za watoto” Alisema Rabikira

Miongoni mwa watoto waliohudhuria maadhimisho hayo kutoka shule mbalimbali,Blo hii ilipata fursa ya kuongea na Aneth George kutoka Kibasila Sekondari pamoja na Adnan Kaizer kutoka
Makongo Sekondari wakielezea jinsi gani wameipokea siku hiyo na mapendekezo yao kwa jamii juu ya haki za watoto


Aneth alisema, Hakizao nilazima zilindwe na kuwa Serikali iteuwe siku moja kwa watoto kujadili haki zao ndani ya Rasimu ya katiba mpya ilinao wajue hakizao zitakazo kuwepo katika kabita mpya. Alisema Aneth

Adnan Kaizer kwa upande wake amesema, suala la wazazi hasa wa kambo kuwatumikisha watoto kinyume na uwezo wao na sheria isemavyo sio haki nakuwa kila mtu awajibike kumlinda mtoto. Aslisema Adnan

Siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa kila mwaka Duniani kote, tarehe 16 June lakini shirika la LHRC limeamua kufanya hii leo. Kimataifa shirika la Kazi Duniani ILO lilitoa ripoti yake kuhusiana na siku hiyo ambapo watoto Milioni 10.5 barani Afrika wanatumikishwa majumbani

MLIPUKO ARUSHA, SERIKALI KUTOA MILIONI 100 KUMPATA MTUHUMIWA



Huku watanzania wakiwa katika hali ya sinto fahamu kutokana na bomu lililolipuka huko Arusha na kujeruhi watu zaidi ya 55 huku watu 3 wakiwa wamefariki hadi hivi sasa kutokana na Bomu hilo



Tayari Serikali imeunda tume kuchunguza tukio hilo, pamoja na kutoa kiasi cha Shulingi Millioni 100 kwa mtu yeyote atakaye toa taarifa za kumkamata mtu ambaye anahusika na tukio hilo ilihatua zaidi ziweze kuchukuliwa



Akiongea mapema leo Bungeni,Waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa Bunge Mhe. William Lukuvi amesema serikali itatoa jumla ya shilingi Milioni 100 kwa yeyote atakaye mtaja aliyehusika na tukio hilo huku akiwasihi watanzania kuwa wamoja na kutokubali kutumiwa na watuwasio kuwa na mema kwa Taifa letu

TAMASHA LA FILAMU NCHINI KUANZA JULAI MOSI 2013 MKOANI MWANZA

Tamasha la Filamu nchini lijulikanalo kama Tanzania Open Film linatarajia kufanyika katika jiji la Mwanza kuanzia Julai mosi mpaka Julai 7 mwaka huu





Akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake Muigizaji Jacob Steven maarufu kama JB amesema hiyo ni nasafi kubwa sana kwa wasanii kwa sababu watapata fursa ya kuonana na mashabiki wao na kuzungumza nao moja kwa moja,


Pia watatumia nafasi hiyo kugawa vyandarua katika Hospitali ya sekoture iliyopo jijini Mwanza ilikuweza kuwasaidia akina mama na watoto katika hospitali hiyo


Meneja wa Habari na mawasiliano wa TBL Edith Mushi amesema, katika miaka miwili iliyopita tangu tamasha hilo kuanza wamejifunza vitu vingi sana kikubwa nikuwa watanzania wengi wanazipenda na kuzikubali Filamu za kitanzania

Aidha Edith, amesema wanaendelea kushirikiana na Sophia Records kuandaa tamasha hilo, Ambapo Mkurugenzi wa kampuni ya Sophia Records bwana Mussa Kissoky amesema waliamua kuanzisha tamasha hilo baada ya kuona kiu ya watanzania kupata fursa ya kukutana na wasanii wao


Hatahivyo, ilifahamika kuwa kutokana na hali yakuwa na vurugu za hapa na pale Tamashahili lilitakiwa kuwa mkoani humo na badala yake likapelekwa mkoani Mwanza


KESI YA BALOZI MZENGI NA BIASHARA YA KUSAFIRISH MWANADAMU, YAHUSISHWA ZIARA YA OBAMA NCHINI TANZANIA

KESI YA BALOZI MZENGI NA BIASHARA YA KUSAFIRISH MWANADAMU, YAHUSISHWA ZIARA YA OBAMA NCHINI TANZANIA

Licha y Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Alfonso Lenhard kutoa sababu ya ziara ya Rais wa Taifa la Marekani, Barack Obama nchini Tanzania haina ajenda ya siri: "kuna maswali mengi naulizwa kwa  nini Rais Obama amechagua kuzuru Tanzania.

Balozi Lenhardt alisema: kuwa"Ni kweli Obama atakuja Tanzania. Lakini niwahakikishie tu kuwa haji kupora rasilimali za Tanzania, huku akitaj sababu nne ambazo ni kutokana na kuwa Tanzania ni mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku. Akasema Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara: 

 
“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani.”
Kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo. Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini na kwamba Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni. 

Kuhimiza haja ya Afrika kutayarisha viongozi wa kizazi kijacho. Ameanzisha programu ya kuandaa viongozi wa kizazi inayoitwa `Young African Leaders Initiative’ na Watanzania watatu, Modesta Lilian Mahiga, Masoud Salim Mohamed na Malula Hassan Nkanyemka walishiriki katika mpango huo na kukutana na kiongozi huyo mwaka 2010: 

Hayayote hayaja waridhisha wachambuzi mbalimbali wa kiasi huku kila mtu kuamini ajuavyo na kwa muono wake yeye,  katika uchambuzi wa Tovuti ya Washington Post huko mrekani mchmbuzi mmoj hajaridhishwa na ziara ya Ris huyo nchini Tanzania huku akiilingnish Tanzania na nchi inyotetea biashara ya binadamu (
 human trafficking. ) kwa kufananisha  tukio alilolifanya blozi wa Tanzani huko Washington bwana Allan S Mzengi dhidi ya  Zipora Mzengo 


Kusoma alichokiandika Dana Milbaank ktika tovuti ya The Washington Post juu y Rais Obama Kuja Tanzania Fungua hap chini kusom zaidi 

http://www.washingtonpost.com/opinions/dana-milbank-obamas-ill-advised-visit-to-tanzania/2013/06/07/397b00fa-cf88-11e2-8845-d970ccb04497_story.html


LORI AINA YA SCANIA LATEKETEA KWA MOTO MBEZI

Jana Majira ya saambili usiku meneo ya Mbezi beach samaki Lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 194 ATR liliungua moto kutokana na tairi la mbele kupata pancha likitokea maeneo ya tegeta

Moto huo uiliteketez eneo lote la mbele laa gari hilo ambalo lilikuwa limebeba mchanga, Kwmujibu w Meja Nurdin mkuu wa kituo cha polisi cha Afrikana, Gari hilo linamilikiwa na kmpuni ya Kilimanjaro Track.


Kikosi cha zima moto kilifika eneo la tukio nakufanikiwa kuzima moto huo kabla gari hilo alija sababisha madharaa makubwa,

Chajabu nikwamba licha yaa wnanchi kuona moto huo ukiwak kwa kasi lakini bado walijazana eneo la tukio huku madereva nao wakikatiza pembeni kabisa ya gari hilo lililokuwa likiendelea kutekete kwa moto

Katika tukio hilo hakuna mtu yeyote aliye ripotiwa kupoteza maisha. 

TUHUMA ZA RUSHWA DHIDI YA NAIBU WAZIRI WA ELIMU ZILIZOTOLEWA NA CHADEMA

TUHUMA ZA RUSHWA DHIDI YA NAIBU WAZIRI WA ELIMU ZILIZOTOLEWA NA CHADEMA

CHADEMA yamnasa Waziri Mulogo kwa rushwa

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemfikisha Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo, mbele ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za kutoa rushwa ya ahadi ya mifuko ya saruji na fedha taslimu 40,000 kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi.

Chama hicho pia kimemfungulia faili la tuhuma za ubakaji mgombea udiwani wa Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mdogo wa kata ya Mbalamaziwa, Zuberi Nyomolela, kwa kosa kuishi kinyumba na binti mwanafunzi.

Hayo yamesemwa jana katika kijiji cha Mbalamaziwa na mwanasheria wa CHADEMA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Sinkara Lucas, kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Mbalamaziwa, uliohudhuriwa na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe.


MILLIONI MIA 320 KUOKOA WANAWAKE WAJAWAZITO, RUKWA NA MWANZA



Serikali imegundua njia mpya yakuwawezesha wanawake kuhudhuria hospitali wakati wakujifungua baada ya kubaini kuwa, Asilimia 98 ya wanawake wanahudhuria kliniki ni asilimia 51 tu kati yao ndio hurudi tena kujifungua katika vituo hivyo

Hayo yamesemwa na Mganga mkuu wa serikali Dr. Donan Mmbando wakati akipokea magari 4 ya wagonjwa yenye dhamani ya shilingi Millioni 32 kutoka kwa shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na huduma za wazazi na mwana la Plan International, magari ambayo yatatumiwa mkoani Rukwa na Mwanza

Kushoto ni Mganga Mkuu wa serikali Dr. Donan Mmbando, katikati ni Mwakilishi wa CIDA Jonathan Arnold, kulia ni David Muthungu kurugenzi wa Plan International

“Idadi kubwa ya wanawake huripoti kliniki lakini wachache sana ndio hurudi kujifungua hospitalini, hii husababishwa na kukosa huduma za kijifungulia, fedha ya matibabu na maamuzi ya kifamilia pengine kutokana na umbali mrefu wa kupata huduma za afya” Alisema Dr Donan

Dr. Donan amesema, Tanzania inajitahidi iliiweze kufanikisha malengo ya Millenia ifikapo mwaka 2015 kwakupunguza vifo vya wanawake wakati wa kujifungua pamoja na vifo vya watoto wachanga baada ya kuzaliwa kutoka asilimia 32 mpaka asilimia 26 kwa watoto.




Vifo vingi vya wanawake hutokana na kutokwa damu nyingi kabla na baada ya kujifungua, Maleria na Anemia, pamoja na Virusi vya ukimwi, kujifungua katika umri mdogo pamoja na sababu nyingine nyingi , lakini kwa watoto wanafariki maratu wanapo zaliwa ni Elfu 45 ndani ya mwaka mmoja. Alisema Dr. Donan

Plan International imebaini kuwa katika mkoa wa Rukwa niasilimia 29 tu ya wanawake ndio huudhuria hospitali wakati wakujifungua wakati mkoani Mwanza ni asilimia 44. hii hutokana na umbali wa huduma za Afya kwa jamii za zijijini katika mikoa hiyo

“Tafiti za Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa asilimia 90 ya watanzania wanakaa kilometa 10 kutoka kilipo kituo cha Afya nahii inachangia kiwango cha juu cha kina mama kujifungua nyumbani” alisema Mkurugenzi wa Plan International bwana David Muthungu



Shirika hilo limetoa msaada wa magari 4 yenye dhamani dola 200,000 ambayo nisawa na shilingi Millioni miatatu na ishirini (320,000,000)  iliyaweze kutumika katika mikoa ya Rukwa na Mwanza ilikuwezesha wanawake kujifungua hospitali na kupunguza vifo wakati wakujifungua

Magari hayo yatawekwa katika vituo vya Afya ilikutoa huduma ya dharura kwa wajawazito na watoto wachanaga katika vituo vya Wampembe na Mtowisa vya Rukwa vijijini na Mwangika na Sangubuye vya Sengerema mwanza. Huku ikikadiriwa kuwa wanawake laki 3 watanufaika na msaada huo.

Kategori

Kategori